-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufunulia Umma Matendo ya Maofisa Wadhalimu
Lilionwa kuwa jambo la kunufaisha kuwajulisha watu katika maeneo fulani juu ya yale ambayo maofisa wa huko walikuwa wakifanya. Katika Quebec, wakati mahakama zilipowatenda Mashahidi kwa njia iliyofanana na ile ya Mabaraza ya Kuwahukumu Wazushi wa Kidini, barua ilipelekwa kwa washiriki wote wa bunge la Quebec ikieleza mambo ya hakika. Hatua ilipokosa kuchukuliwa, Sosaiti ilipeleka nakala ya barua hiyo kwa wafanya-biashara 14,000 kotekote mkoani. Kisha habari hiyo ikapelekwa kwa wahariri wa magazeti ya habari ili ichapwe.
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Gestapo waliongeza jitihada zao za kukomesha utendaji wa Mashahidi wa Yehova. Baada ya wengi kukamatwa katika 1936, walifikiri kwamba labda walikuwa wamefanikiwa. Lakini mnamo Desemba 12, 1936, Mashahidi kama 3,450 ambao bado walikuwa huru katika Ujerumani waligawanya upesi nchini kote azimio lililochapwa lililoonyesha wazi kusudi la Yehova na likaonyesha uamuzi wa Mashahidi wa Yehova wa kumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu. Wapinzani hawangeweza kuelewa ni kwa njia gani ugawanyaji huo uliwezekana. Miezi michache baadaye, wakati Gestapo walipopuuza mashtaka yaliyofanywa katika azimio hilo, Mashahidi wa Yehova walitayarisha barua ya wazi ambamo kwayo walitaja waziwazi majina ya maofisa wa Nazi waliokuwa wamewatenda kikatili Mashahidi wa Yehova. Katika 1937, barua hiyo pia iligawanywa sana katika Ujerumani. Hivyo matendo ya watu waovu yalifunuliwa ili watu wote waone. Hilo liliwapa umma fursa ya kuamua ni mwendo gani ambao wao binafsi wangefuata kuhusu watumishi hao wa Aliye Juu Zaidi.—Linganisha Mathayo 25:31-46.
Utangazaji wa Duniani Pote Waleta Kitulizo Kidogo
Serikali nyingine pia zimewatendea kikatili Mashahidi wa Yehova, zikikataza mikutano yao na mahubiri ya hadharani. Katika visa fulani serikali hizo zimefanya Mashahidi wakafukuzwa kazini kwa nguvu na watoto wao wakazuiwa kwenda shuleni. Idadi fulani ya serikali pia zimetumia ukatili wa kimwili. Na bado, mara nyingi nchi hizohizo zina katiba inayohakikishia uhuru wa ibada. Kwa kusudi la kuleta kitulizo kwa ndugu zao wanaonyanyaswa, mara nyingi Watch Tower Society imejulisha waziwazi ulimwenguni pote mambo mengi kuhusu mnyanyaso huo. Hayo hufanywa kupitia magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na nyakati nyingine ripoti hizo hutumiwa na waandishi wa magazeti. Kisha maelfu mengi ya barua za kutoa maombi kwa niaba ya Mashahidi hufurika ndani ya ofisi za maofisa wa serikali kutoka kotekote ulimwenguni.
Kama tokeo la kampeni kama hiyo katika 1937, gavana wa Georgia, katika Marekani alipokea barua zipatazo 7,000 kutoka nchi nne katika kipindi cha siku mbili, na meya wa La Grange, Georgia, pia aligharikishwa na maelfu ya barua. Kampeni kama hizo zilifanywa vilevile kwa niaba ya Mashahidi wa Yehova nchini Argentina katika 1978 na 1979, Benin katika 1976, Burundi katika 1989, Ethiopia katika 1957, Gabon katika 1971, Hispania katika 1961 na tena katika 1962, Jamhuri ya Dominika katika 1950 na 1957, Kamerun katika 1970, Malawi katika 1968, 1972, 1975, na tena katika 1976, Maleya katika 1952, Msumbiji katika 1976, Singapore katika 1972, Swaziland katika 1983, Ugiriki katika 1963 na 1966, Ureno katika 1964 na 1966, pia Yordani katika 1959.
Kielelezo cha hivi karibuni cha yale yanayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote ili kuleta kitulizo kwa ndugu zao wanaoonewa, ni hali katika Ugiriki. Kwa sababu ya mnyanyaso mwingi wa Mashahidi wa Yehova wenye kuchochewa na makasisi wa Orthodoksi ya Ugiriki huko, magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! pia (ambayo yana mwenezo wa ujumla wa kimataifa zaidi ya nakala 22,000,000) yaliripoti mambo mengi kuhusu mnyanyaso huo katika 1986. Mashahidi katika nchi nyinginezo waliombwa wawaandikie maofisa wa serikali ya Ugiriki kwa niaba ya ndugu zao. Wao walifanya hivyo; na kama ilivyoripotiwa katika gazeti la habari la Athens Vradyni, waziri wa sheria aligharikishwa na barua zaidi ya 200,000 kutoka nchi zaidi ya 200 na katika lugha 106.
-