Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwimbieni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 15
    • Baada ya kuwekwa kuwa mfalme wa Israeli, Daudi alipanga ili utumishi wa maskani utie ndani muziki mtamu. Zaidi ya asilimia kumi ya Walawi wote waliotumika katika maskani, yaani, Walawi 4,000, walipewa mgawo wa “kutoa sifa,” na 288 ‘walizoezwa nyimbo kwa Yehova, wote wakiwa wajuzi.’—1 Nya. 23:3, 5; 25:7.

      4 Daudi mwenyewe alitunga nyimbo nyingi kati ya zile ambazo Walawi waliimba. Ni wazi kwamba Waisraeli wote ambao walipata pendeleo la kuwapo wakati zaburi za Daudi zilipoimbwa waliguswa moyo sana na nyimbo walizosikia. Baadaye, sanduku la agano lilipoletwa Yerusalemu, ‘Daudi aliwaambia wakuu wa Walawi wawaweke ndugu zao waimbaji wakiwa na vyombo vya nyimbo, vinanda na vinubi na matoazi, wakipiga kwa sauti ili sauti ya kushangilia itokee.’—1 Nya. 15:16.

      5, 6. (a) Kwa nini muziki ulikaziwa sana uangalifu wakati wa utawala wa Daudi? (b) Tunajua jinsi gani kwamba katika Israeli la kale muziki ulionwa kuwa wa maana katika ibada?

      5 Kwa nini muziki ulikaziwa sana uangalifu katika siku za Daudi? Je, ni kwa sababu tu mfalme alikuwa mwanamuziki? Hapana, kulikuwa na sababu nyingine ambayo ilifunuliwa karne nyingi baadaye wakati Mfalme Hezekia aliyekuwa mwadilifu alipoanzisha tena utumishi katika hekalu. Tunasoma hivi katika andiko la 2 Mambo ya Nyakati 29:25: “Akawaweka [yaani, Hezekia] Walawi katika nyumba ya Yehova, wakiwa na matoazi, na vinanda na vinubi, kulingana na amri ya Daudi na ya Gadi mwonaji wa mfalme na ya nabii Nathani, kwa maana amri hiyo ilikuwa kulingana na mkono wa Yehova kupitia manabii wake.”

      6 Ndiyo, kupitia manabii wake, Yehova aliwaagiza waabudu wake wamsifu kwa nyimbo. Pia, waimbaji kutoka katika kabila la kikuhani hawakupewa migawo ambayo Walawi wengine walitakiwa wafanye ili wawe na wakati wa kutosha wa kutunga nyimbo na inaelekea sana, ili pia wafanye mazoezi.—1 Nya. 9:33.

      7, 8. Ni jambo gani ambalo ni la maana zaidi kuliko ustadi inapohusu kuimba nyimbo zetu za Ufalme?

      7 Huenda ukasema, “Inapohusu muziki, bila shaka siwezi kuhesabiwa kuwa kati ya waimbaji stadi ambao waliimba katika maskani!” Lakini si wanamuziki wote Walawi waliokuwa waimbaji stadi. Kulingana na andiko la 1 Mambo ya Nyakati 25:8, kulikuwa pia na ‘wenye kujifunza.’ Pia, ni vizuri kukumbuka kwamba huenda kulikuwa na wanamuziki na waimbaji fulani ambao walikuwa stadi sana kutoka katika makabila mengine ya Israeli, lakini Yehova aliwapa Walawi mgawo wa kushughulikia muziki. Tunaweza kuwa na hakika kwamba iwe walikuwa ‘wajuzi,’ yaani, waimbaji stadi, au ‘wenye kujifunza,’ Walawi wote waaminifu walitimiza kazi hiyo kwa moyo wote.

  • Mwimbieni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi—2010 | Desemba 15
    • 9. Eleza mambo ambayo huenda ungeona na kusikia ikiwa ungehudhuria sherehe ya kuzindua hekalu wakati wa utawala wa Sulemani.

      9 Wakati wa utawala wa Sulemani, muziki ulitimiza sehemu ya maana katika ibada safi. Wakati wa kuzinduliwa kwa hekalu, kulikuwa na kikundi kamili cha kupiga muziki, na kilitia ndani watu 120 waliopiga tarumbeta. (Soma 2 Mambo ya Nyakati 5:12.) Biblia inatuambia kwamba ‘wapiga-tarumbeta [ambao wote walikuwa makuhani] na waimbaji walikuwa kama mtu mmoja kwa kutokeza sauti moja isikike katika kumsifu na kumshukuru Yehova, “kwa maana yeye ni mwema, kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki