-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha MalakiMnara wa Mlinzi—2007 | Desemba 15
-
-
MAKUHANI ‘WAMESABABISHA WENGI WAJIKWAE’
Yehova anaonyesha hisia zake kuelekea Israeli kwa kusema hivi: “Nimewapenda ninyi.” Lakini makuhani wamelidharau jina la Mungu. Kwa njia gani? “Kwa kutoa juu ya madhabahu [yake] mkate uliotiwa unajisi,” na kwa kutoa “mnyama kilema au mgonjwa” kwa ajili ya dhabihu.—Malaki 1:2, 6-8.
Makuhani ‘wamesababisha wengi wajikwae katika sheria.’ Watu ‘wanatendeana kwa hila.’ Wengine wamechukua wake wa kigeni. Na wengine wao wamewatendea hila ‘wake wa ujana wao.’—Malaki 2:8, 10, 11, 14-16.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha MalakiMnara wa Mlinzi—2007 | Desemba 15
-
-
“BWANA WA KWELI ATAKUJA KWENYE HEKALU LAKE”
“Kwa ghafula Bwana wa kweli [Yehova Mungu] atakuja kwenye hekalu Lake,” na “mjumbe wa agano [Yesu Kristo].” Mungu ‘atawakaribia watu wake ili kuwahukumu,’ naye atakuwa shahidi wa haraka juu ya watenda mabaya wote. Zaidi ya hayo, “kitabu cha kumbukumbu” kitaandikwa kwa ajili ya wale wanaomwogopa Yehova.—Malaki 3:1, 3, 5, 16.
Siku ambayo “inawaka kama tanuru” itakuja na kuwateketeza waovu wote. Kabla ya siku hiyo kuja, nabii atatumwa ili ‘kugeuza mioyo ya akina baba irudi kwa wana, na mioyo ya wana irudi kwa akina baba.’—Malaki 4:1, 5, 6.
-