-
“Katika Hatari za Baharini”Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
KATIKA giza la usiku, meli inayobeba watu 276 yakaribia kisiwa kimoja katika Mediterania. Wanabaharia na abiria wamechoka kwa kurushwa huku na huku katika maji yenye dhoruba kwa siku 14. Wanapoona ghuba wakati wa mapambazuko, wanajaribu kupeleka chombo hicho pwani. Lakini omo yasakama kiasi cha kutoweza kusonga, na mawimbi yavunja tezi vipande vipande. Wote kwenye meli hiyo waiacha na wafaulu kufika kwenye fuo za Malta kwa kuogelea au kwa kushikilia kwa nguvu mbao na vitu vingine. Wakiwa wamepata baridi na kuchoka, wanajivuta kutoka katika mawimbi hayo yaliyochafuka. Paulo, mtume Mkristo, yuko miongoni mwa abiria hao. Anasafirishwa hadi Roma ili kufanyiwa kesi.—Matendo 27:27-44.
-
-
“Katika Hatari za Baharini”Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Ni jambo gani linaloweza kusemwa kuhusu meli iliyovunjikia Malta ambayo Paulo alikuwa amepanda? Ilikuwa meli ya nafaka, “mashua kutoka Aleksandria ikisafiri kuelekea Italia.” (Matendo 27:6, New World Translation of the Holy Scriptures—With References, kielezi-chini) Makundi ya meli za nafaka yalimilikiwa kibinafsi na Wagiriki, Wafoinike, na Wasiria, walioziongoza na kuziandalia vifaa. Hata hivyo, meli hizo zilikodiwa na Serikali. “Kama ilivyokuwa katika kukusanya kodi,” asema mwanahistoria William M. Ramsay, “serikali iliona kuwa ni rahisi kuwapa wanakandarasi kazi hiyo kuliko kujipangia watu na vifaa vingi sana vilivyohitajika kwa utumishi huo mkubwa.”
-
-
“Katika Hatari za Baharini”Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Chombo kilichovunjika Paulo akiwamo huko Malta pia kingeonwa kuwa kikubwa. Meli ya aina hiyo ingeweza kuwa kubwa kadiri gani?
Maandishi fulani yalisababisha msomi mmoja kusema hivi: “[Meli] iliyo ndogo zaidi ambayo ingewafaa watu wa zamani ilikuwa yenye tani 70 hadi 80. Meli yenye ukubwa uliopendwa zaidi, angalau katika enzi ya Ugiriki, ilikuwa yenye uzito wa tani 130. Meli yenye uzito wa tani 250, ingawa ilionekana mara nyingi, kwa hakika ilikuwa kubwa kupita wastani. Katika nyakati za Roma meli zilizotumiwa katika utumishi wa usafirishaji wa kifalme zilikuwa kubwa hata zaidi, ukubwa uliopendwa ulikuwa tani 340. Meli kubwa zaidi zilizosafiri baharini zilifikia uzito wa tani 1300, au labda kubwa zaidi kuliko hizo.” Kulingana na ufafanuzi ulioandikwa katika karne ya pili W.K., meli ya kubeba nafaka Isis ya Aleksandria ilikuwa yenye urefu wa meta 55, na yenye upana wa karibu meta 14, na ngama yenye kina cha meta 13 hivi, na huenda ingeweza kubeba tani zaidi ya elfu moja za nafaka na labda abiria mia kadhaa.
-
-
“Katika Hatari za Baharini”Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 15
-
-
Kwa wazi, Paulo alijua hatari za kusafiri baharini wakati wa majira yasiyofaa. Hata alitoa shauri dhidi ya kusafiri mwisho-mwisho wa Septemba au mapema Oktoba, akisema hivi: “Wanaume, nahisi kwamba uendeshaji utakuwa na dhara na hasara kubwa si ya shehena na mashua tu bali pia ya nafsi zetu.” (Matendo 27:9, 10) Hata hivyo, ofisa-jeshi aliyeshika usukani akayapuuza maneno hayo, na jambo hilo likatokeza kuvunjikiwa meli huko Malta.
-