-
Kuwa na Adabu Nzuri Ni Sifa ya Watu wa MunguHuduma ya Ufalme—2001 | Agosti
-
-
Kuwa na Adabu Nzuri Ni Sifa ya Watu wa Mungu
1 Leo si rahisi kuona adabu nzuri. Kwa nini? Watu wana haraka sana hivi kwamba mara nyingi hawafikirii matendo ya kawaida ya kiungwana kama vile kusema “Tafadhali,” “Asante,” au “Kunradhi.” Neno la Mungu lilitabiri kwamba siku za mwisho adabu zingeendelea kuharibika. Neno lake lilisema kwamba watu wangekuwa ‘wenye kujipenda wenyewe, wenye kujitanguliza, wenye kiburi, wasio na shukrani, wasio na shauku ya kiasili, wasio na hali ya kujidhibiti, wasio na upendo wa wema, na wenye vichwa vigumu.’ (2 Tim. 3:1-4) Sifa zote hizo ni ukosefu wa adabu. Wakiwa watu wa Mungu, lazima Wakristo wajihadhari ili wasiwe kama ulimwengu huu usiowaheshimu wengine.
2 Adabu Ni Nini? Adabu nzuri yaweza kufafanuliwa kuwa kutambua sana hisia za wengine, uwezo wa kuishi na wengine kwa amani. Sifa za adabu nzuri ni ufikirio, uungwana, fadhili, upole, busara na kujali. Sifa hizo zinatokana na upendo wa mtu kwa Mungu na kwa jirani yake. (Luka 10:27) Sifa hizo hazigharimu chochote, lakini zina thamani sana katika kuboresha uhusiano wetu na wengine.
3 Yesu Kristo aliweka kielelezo bora kabisa. Sikuzote alidhihirisha ile Kanuni Bora: “Kama vile mtakavyo watu wawafanyie nyinyi, wafanyieni wao kwa njia hiyohiyo.” (Luka 6:31) Je, sisi hatustaajabu jinsi Yesu alivyowajali na kuwapenda wanafunzi wake? (Mt. 11:28-30) Adabu yake njema haikutokana na sheria zilizoandikwa kwenye vitabu vya adabu nzuri. Zilitokana na moyo mnyoofu na mkarimu. Lazima tujaribu kumwiga.
4 Ni wakati gani ambapo Wakristo wanahitaji kuwa na adabu nzuri? Je, ni wakati wa vipindi vya pekee tu, wakati wanataka kujionyesha kuwa eti ni wazuri? Je, ni wakati tu wa kujaribu kuwavuta wengine? La! Twahitaji kuwa na adabu nzuri nyakati zote.
-
-
Kuwa na Adabu Nzuri Ni Sifa ya Watu wa MunguHuduma ya Ufalme—2001 | Agosti
-
-
14 Adabu Nzuri Ni Muhimu: Kujizoeza tabia za Kikristo hakuletei sifa huduma yetu tu, bali pia huendeleza uhusiano mzuri pamoja na wengine. (2 Kor. 6:3, 4, 6) Tukiwa waabudu wa Mungu mwenye furaha, yapaswa iwe rahisi kwetu kutabasamu, tuwe na utu wenye kupendeza na hata kufanya mambo madogo-madogo yenye fadhili ambayo huwaletea wengine shangwe. Sifa hizo zitapamba maisha yetu tukiwa watu wa Mungu.
-