-
Maswali Kutoka Kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
-
-
Mwanamume na mwanamke ambao hawajafunga ndoa na wanaojifunza Biblia wanataka kubatizwa, lakini hawawezi kuhalalisha muungano wao kwa sababu mwanamume anaishi nchini kinyume cha sheria. Serikali hairuhusu mgeni anayeishi nchini kinyume cha sheria afunge ndoa. Je, wanaweza kutia sahihi Kiapo cha Uaminifu na kisha kubatizwa?
Huenda kufanya hivyo kukaonekana kuwa ni suluhisho, lakini si njia ya Kimaandiko ya kutatua tatizo lao.
-
-
Maswali Kutoka Kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2012 | Desemba 15
-
-
Kwa kuwa hawaelewi maana ya Kiapo cha Uaminifu, watu fulani wanaoishi katika nchi ambazo zinaruhusu talaka, wameuliza ikiwa wanaweza kutia sahihi hati hiyo ili waepuke matatizo au usumbufu.
Katika kisa kilichozungumziwa mwanzoni, mwanamume na mwanamke wanaoishi pamoja katika njia isiyo ya kiadili wanataka kufunga ndoa. Kila mmoja wao yuko huru Kimaandiko; wote hawajafungwa na mwenzi wa zamani. Hata hivyo, mwanamume anaishi nchini kinyume cha sheria, na serikali haiwezi kumruhusu mgeni anayeishi nchini kinyume cha sheria afunge ndoa. (Katika nchi nyingi serikali inaweza kuruhusu ndoa hata kama mmoja wao au wote wawili hawaishi kihalali nchini.) Katika kisa tunachozungumzia, nchi inaruhusu talaka. Kwa hiyo, hakuna sababu ya kutia sahihi Kiapo cha Uaminifu. Kumbuka wenzi hao si kwamba yeyote kati yao alihitaji kumtaliki mwenzi wa zamani, bali wanazuiwa kuoana. Wote wawili wako huru kufunga ndoa. Lakini kwa kuwa mwanamume huyo anaishi kinyume cha sheria nchini, watawezaje kufunga ndoa? Huenda wakahitaji kwenda nchi nyingine ambayo inamruhusu mwanamume huyo kufunga ndoa. Au huenda ikawezekana kufunga ndoa katika nchi wanamoishi kwa sasa ikiwa mwanamume atachukua hatua za kuhalalisha hati zake za kuishi nchini.
Naam, wenzi hao wanaweza kupatanisha maisha yao na viwango vya Mungu na sheria ya Kaisari. (Marko 12:17; Rom. 13:1) Inatazamiwa kwamba watafanya hivyo. Kisha, wanaweza kustahili kubatizwa.—Ebr. 13:4.
-