-
NdoaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ndoa ni mpango wa Mungu. Inawezesha kuwepo uhusiano wa karibu sana kati ya mume na mke pamoja na hisia ya usalama kwa sababu kuna upendo na kwa sababu ya wajibu wa kibinafsi ambao umefanywa na kila mmoja wa wenzi hao. Alipokuwa akiianzisha ndoa, Yehova alifanya hivyo ili kumwandalia mwanamume mwenzi wa karibu ambaye angekuwa kikamilisho chake na pia kuanzisha njia ambayo wanadamu wangeweza kuzaana katika mpango wa familia.
-
-
NdoaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Adamu na Hawa walipoanza kuishi pamoja, je, kulikuwa na “utaratibu wowote wa kisheria”?
Mwa. 2:22-24: “Yehova Mungu akaufanya ubavu ambao alikuwa ameuchukua kutoka kwa mwanamume [Adamu] kuwa mwanamke na kumleta kwa huyo mwanamume. Ndipo huyo mwanamume akasema: ‘Mwishowe huyu ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu. Huyu ataitwa Mwanamke, kwa sababu huyu alitolewa katika mwanamume.’ Hiyo ndiyo sababu mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake nao watakuwa mwili mmoja.” (Ona kwamba Yehova Mungu mwenyewe, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, ndiye aliyewaunganisha Adamu na Hawa. Mwanamume wala mwanamke hawakujiamulia kuishi pamoja bila kujali mamlaka ya kisheria. Ona, pia, jinsi Mungu alivyokazia kudumu kwa muungano huo.)
Mwa. 1:28: “Mungu akawabariki [Adamu na Hawa] na Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, mjaze dunia na kuitiisha, na mtawale samaki wa baharini na viumbe vinavyoruka vya mbinguni na kila kiumbe hai kinachotambaa juu ya dunia.’” (Muungano huo ulibarikiwa na Yule mwenye mamlaka kuu ya kisheria, nao waliruhusiwa kuwa na uhusiano wa kingono, wakapewa kazi ambayo ingefanya maisha yao yawe na kusudi.)
-