-
Unaweza Kupata Furaha Katika Familia IliyogawanyikaMnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
-
-
11 Mifano mingi leo inaonyesha umuhimu wa kufuata shauri la Petro. Fikiria mfano wa Selma. Alipoanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova, mume wake, Steve, hakufurahia. Mume wake anakiri hivi: “Nilikasirika, nikawa na wivu, nikamnyima uhuru nikiogopa kwamba ataniacha.” Selma anasema hivi: “Hata kabla sijapata kweli, haikuwa rahisi kuishi na Steve. Alikuwa na hasira kali. Nilipoanza kujifunza Biblia, hasira yake iliongezeka.” Ni nini kilichosaidia?
12 Selma anakumbuka somo ambalo alijifunza kutoka kwa Shahidi aliyemfundisha Biblia. Selma anasema, “Siku moja, sikutaka kujifunza Biblia. Usiku uliotangulia, Steve alinipiga nilipojaribu kumthibitishia jambo fulani, na nilihuzunika na kujisikitikia. Baada ya kumwambia dada huyo jambo lililotukia na jinsi nilivyohisi, aliniomba nisome andiko la 1 Wakorintho 13:4-7. Nilipokuwa nikilisoma, nilianza kusema, ‘Steve hanitendei kamwe jambo lolote kati ya mambo haya yanayoonyesha upendo.’ Lakini dada huyo akanisaidia kufikiri kwa njia tofauti kwa kuniuliza, ‘Ni mambo mangapi kati ya mambo haya yanayoonyesha upendo ambayo wewe unamtendea mume wako?’ Nilimjibu hivi: ‘Hakuna, kwa kuwa ni vigumu sana kuishi naye.’ Dada huyo akasema hivi kwa upole, ‘Selma, ni nani anayejaribu kuwa Mkristo kati yenu? Ni wewe au ni Steve?’ Nilipotambua kwamba nilihitaji kubadili njia yangu ya kufikiri, nilisali kwa Yehova ili anisaidie kumtendea Steve kwa njia ya upendo zaidi. Pole kwa pole, mambo yakaanza kubadilika.” Baada ya miaka 17, Steve alikubali kweli.
-
-
Unaweza Kupata Furaha Katika Familia IliyogawanyikaMnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
-
-
Mume fulani nchini Nigeria ambaye alikubali kweli miaka 13 baada ya mke wake kuukubali anasema hivi: “Nilipokuwa nikisafiri na Shahidi mmoja, gari lake liliharibika. Aliwatafuta Mashahidi wengine katika kijiji cha karibu, nao wakatupatia mahali pa kulala usiku huo. Walitutunza kana kwamba tulifahamiana tangu utotoni. Mara moja, niliona upendo wa Kikristo ambao mke wangu alikuwa akizungumzia sikuzote.”
-
-
Unaweza Kupata Furaha Katika Familia IliyogawanyikaMnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
-
-
Mume mwingine katika nchi hiyo ambaye mwishowe alikuja kuwa Shahidi anasema: “Akina ndugu na dada walikuwa wakitutembelea, au walitualika katika nyumba zao, na niligundua kwamba wanajali. Hilo lilionekana wazi hasa nilipokuwa nimelazwa hospitalini, wengi wao walikuja kunitembelea.”
-
-
Unaweza Kupata Furaha Katika Familia IliyogawanyikaMnara wa Mlinzi—2012 | Februari 15
-
-
Mume mmoja ambaye zamani hakuwa mwamini alisema hivi: “Mwenzi wa ndoa ambaye ni mwamini anapoanza kuonyesha sifa hizo nzuri, hujui zitagusa jinsi gani akili na moyo wa mwenzi asiye mwamini. Basi usikate tamaa kamwe unaposhughulika na mwenzi wako asiye mwamini.”
-