Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
    • Kuvumilia Mateso na Msiba

      Ni nini kilichompata Yosefu, baba wa kambo wa Yesu? Baada ya kutajwa kifupi katika tukio hilo Yesu alipokuwa kijana, Yosefu hatajwi tena katika vitabu vya Injili. Watu fulani wanafikiri kwamba hilo linaonyesha Yosefu alikufa muda fulani kabla ya huduma ya Yesu kuanza.c Vyovyote vile, inaonekana kwamba kufikia mwisho wa huduma ya Yesu, Maria alikuwa mjane. Alipokuwa akielekea kufa, Yesu alimkabidhi mtume Yohana jukumu la kumtunza mama yake. (Yohana 19:26, 27) Ikiwa Yosefu angekuwa bado hai, huenda Yesu hangefanya hivyo.

      Maria na Yosefu walikuwa wamepitia mambo mengi sana pamoja! Walikuwa wametembelewa na malaika, wakahepa mtawala mkatili, wakahama mara kadhaa, na wakazaa watoto wengi. Ni mara ngapi walipoketi pamoja jioni na kuzungumza kuhusu Yesu, wakijiuliza atakabili mambo gani wakati ujao, na kujiuliza ikiwa walikuwa wakimzoeza na kumtayarisha kwa njia inayofaa? Kisha ghafula Maria alijikuta peke yake.

      Je, umempoteza mwenzi wako katika kifo? Je, bado unahisi uchungu na upweke unaoletwa na msiba huo, hata baada ya miaka mingi? Bila shaka Maria alifarijiwa na imani yake na ujuzi wa kwamba kutakuwa na ufufuo.d (Yohana 5:28, 29) Hata hivyo, mawazo hayo yenye kufariji hayakumwondolea Maria matatizo yake. Kama ilivyo na akina mama wengi wasio na wenzi wa ndoa, Maria alikuwa na daraka gumu la kutunza watoto wake bila msaada wa mume.

      Ni jambo linalopatana na akili kuamini kwamba Yesu alichukua daraka la kuiandalia familia mahitaji Yosefu alipokufa. Ndugu za Yesu walipoendelea kukua wangekubali daraka la kuiandalia familia mahitaji.

  • Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
    • c Imeonekana kwamba kutotajwa tena kwa Yosefu katika masimulizi ya huduma ya Yesu ni jambo lenye kutokeza kwa sababu washiriki wengine wa familia ya Yesu, yaani, mama, ndugu na dada zake wanatajwa. Kwa mfano, katika karamu ya arusi huko Kana, Maria anatajwa na hata inaonekana alikuwa na daraka fulani, lakini Yosefu hatajwi. (Yohana 2:1-11) Katika kisa kingine, tunaona watu katika mji wa nyumbani wa Kristo wakimtaja Yesu kuwa “mwana wa Maria” wala si mwana wa Yosefu.—Marko 6:3.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki