-
Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
-
-
Mke na Mama Mwenye Bidii
Mbali na masimulizi ya kuzaliwa na maisha ya utotoni ya Yesu, Maria hatajwi sana katika vitabu vya Injili. Hata hivyo, tunajua kwamba Maria na Yosefu walikuwa na angalau watoto wengine sita. Huenda ukashangazwa na hilo. Lakini fikiria yale ambayo vitabu vya Injili vinasema.
Yosefu aliheshimu sana pendeleo la Maria la kubeba mimba ya Mwana wa Mungu. Kwa hiyo, aliepuka kufanya ngono naye kabla Yesu hajazaliwa. Mathayo 1:25 inasema kwamba Yosefu “hakufanya ngono naye mpaka alipozaa mwana.” Neno “mpaka” katika mstari huo linaonyesha kwamba baada ya Yesu kuzaliwa, Yosefu na Maria walifanya ngono kama mke na mume. Vitabu vya Injili vinasema kwamba kwa sababu hiyo Maria na Yosefu walipata watoto, wana na mabinti. Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yudasi walikuwa ndugu wa kambo wa Yesu. Alikuwa na angalau mabinti wawili. (Mathayo 13:55, 56) Hata hivyo, mimba za watoto hao zilitungwa kwa njia ya kawaida.b
-
-
Mfano wa Maria Unatufundisha Nini?Mnara wa Mlinzi—2009 | Januari 1
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 6]
Je, Yesu Alikuwa na Ndugu na Dada?
Ndiyo, alikuwa nao. Wanatheolojia fulani wamejaribu kuupinga ukweli huo hata ingawa vitabu vya Injili vinathibitisha jambo hilo mara kadhaa. (Mathayo 12:46, 47; 13:54-56; Marko 6:3) Hata hivyo, wasomi wa Biblia wametoa hoja mbili kuhusu nadharia za kwamba Maria hakupata watoto wengine. Kwanza, nadharia hizo zinachochewa na fundisho la kanisa lililotokea baadaye, yaani, Maria alibaki bikira maisha yake yote. Pili, nadharia hizo haziwezi kuthibitishwa.
Kwa mfano, nadharia moja inadokeza kwamba “ndugu” wanaotajwa walikuwa ndugu wa kambo, yaani, wana ambao Yosefu alipata katika ndoa ya mapema. Wazo hilo halina msingi kwa sababu lingemfanya Yesu asiwe na haki ya kisheria ya mzaliwa wa kwanza ya kurithi kiti cha ufalme cha Daudi.—2 Samweli 7:12, 13.
Nadharia nyingine inasema kwamba ndugu hao walikuwa binamu za Yesu, ingawa Maandiko ya Kigiriki yanatumia maneno tofauti kwa ajili ya “ndugu,” “binamu,” na “mtu wa ukoo.” Kwa hiyo, msomi Frank E. Gaebelein anasema kuwa nadharia hizo za kidini ni mawazo ya kubuniwa. Anamalizia kwa kusema: “Njia ya kawaida ya kuelewa neno ‘ndugu’ . . . ni kwamba neno hilo linarejelea wana wa Maria na Yosefu na hivyo wao ni ndugu za Yesu wa mama mmoja.”
-