Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoa Kunakompendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Juni 1
    • Nyumba ya mwanamke mmoja Mkristo mwenye umri mkubwa ilikuwa imeharibika sana. Aliishi peke yake na hakuwa na familia ya kumsaidia. Kwa miaka mingi, mikutano ya Kikristo ilifanyiwa nyumbani mwake, na mara nyingi aliwaalika watu kwa mlo. (Matendo 16:14, 15, 40) Watu wa kutaniko walijitolea kumsaidia walipoona uhitaji wake. Wengine walitoa pesa na wengine wakajitolea kufanya kazi. Kwa miisho-juma kadhaa, wajitoleaji walijenga paa jipya, choo na bafu mpya, wakapiga plasta na kupaka rangi orofa ya kwanza, kisha wakatengeneza makabati mapya jikoni. Mbali na kumsaidia mwanamke huyo, utoaji wao ulileta umoja kutanikoni na majirani walivutiwa kuona jinsi Wakristo wa kweli wanavyotoa.

  • Kutoa Kunakompendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Juni 1
    • Mashahidi wa Yehova leo huwa tayari kusaidia misiba inapotokea. Kwa mfano, wakati wa kiangazi mwaka wa 2001, dhoruba ilisababisha mafuriko makubwa huko Houston, Texas, Marekani. Nyumba nyingi ziliharibiwa vibaya sana na jumla ya nyumba 723 za Mashahidi ziliharibiwa kwa kiasi fulani. Halmashauri ya kutoa misaada yenye wazee Wakristo wenye uzoefu iliundwa mara moja ili kuchunguza mahitaji ya kila mtu na kutoa pesa za kusaidia Mashahidi hao wakabiliane na hali na kurekebisha nyumba zao. Wajitoleaji kutoka kwenye makutaniko jirani walifanya kazi yote. Shahidi mmoja alithamini sana msaada huo hivi kwamba alipopokea malipo ya bima ya kurekebisha nyumba yake, alitoa pesa hizo mara moja kwa hazina ya misaada ili kuwasaidia wengine wenye uhitaji.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki