-
2. Dumisha UsafiAmkeni!—2012 | Juni
-
-
● Usiweke nyama mbichi pamoja.
Ili kuzuia kuenea kwa bakteria pakia vizuri nyama mbichi ya ng’ombe, kuku, na samaki, na uiweke mbali na vyakula vingine. Tumia ubao tofauti kukatia vyakula hivyo au uoshe ubao huo kwa sabuni na maji moto kabla na baada ya kukatia nyama mbichi au samaki.
-
-
3. Tayarisha na Uhifadhi Chakula VizuriAmkeni!—2012 | Juni
-
-
● Nyama iliyoganda isiyeyushwe nje ya friji.
Wizara ya Kilimo ya Marekani inasema kwamba “hata ingawa sehemu ya katikati ya nyama huwa bado imeganda inapoyeyuka nje ya friji, huenda sehemu ya nje ya nyama hiyo ikawa na joto la kati ya nyuzi 4 Selsiasi na nyuzi 60 Selsiasi, kiwango kinachosemwa kuwa hatari kwa sababu bakteria huongezeka haraka.” Badala yake, yeyusha chakula ndani ya friji, kwenye mikrowevu, au kitumbukize ndani ya maji baridi kikiwa kimepakiwa.
-