-
Mlo wa Jioni wa Bwana Una Maana Gani Kwako?Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 15
-
-
Wahudhuria Wakiwa Watazamaji Wenye Heshima
6. Mungu amewapa nani pendeleo la kushiriki Mlo wa Jioni wa Bwana?
6 Je, wale wanaowafanyia mema mabaki ya ndugu za Kristo 144,000 wanapaswa kushiriki kula Mlo wa Jioni wa Bwana? (Mathayo 25:31-40; Ufunuo 14:1) La. Mungu amewapa pendeleo hilo watu ambao amewatia mafuta kwa roho takatifu ili wawe “warithi-washirika pamoja na Kristo.” (Waroma 8:14-18; 1 Yohana 2:20) Basi wale wanaotumaini kuishi milele katika paradiso duniani chini ya utawala wa Ufalme wana pendeleo gani? (Luka 23:43; Ufunuo 21:3, 4) Wao huhudhuria Ukumbusho wakiwa watazamaji wenye heshima kwa kuwa wao si warithi-washirika pamoja na Yesu wenye tumaini la kwenda mbinguni.—Waroma 6:3-5.
-
-
Mlo wa Jioni wa Bwana Una Maana Gani Kwako?Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 15
-
-
Kuwatafuta “Kondoo Wengine”
9. Maoni kuhusu “umati mkubwa” yalirekebishwaje mwaka wa 1935, na hilo liliwaathirije baadhi ya watu waliokuwa wakishiriki mifano ya Ukumbusho hapo awali?
9 Muda si muda, tengenezo la Yehova lilianza kukazia fikira jamii nyingine mbali na wafuasi watiwa-mafuta wa Kristo. Jambo muhimu sana kuhusiana na jamii hiyo lilitukia katikati ya miaka ya 1930. Hapo awali, watu wa Mungu walifikiri kwamba “umati mkubwa” unaotajwa kwenye Ufunuo 7:9 ni jamii ya pili ya kiroho ambayo ingeungana na watiwa-mafuta 144,000 waliofufuliwa na kwenda mbinguni—wakiwa waandamani wa bibi-arusi wa Kristo. (Zaburi 45:14, 15; Ufunuo 7:4; 21:2, 9) Lakini hotuba iliyotolewa kwenye kusanyiko la Mashahidi wa Yehova huko Washington, D.C., Marekani mnamo Mei 31, 1935, ilieleza kupitia Maandiko kwamba “umati mkubwa” (“mkutano mkubwa,” Union Version) ni “kondoo wengine” wanaoishi katika nyakati za mwisho. (Yohana 10:16) Baada ya kusanyiko hilo, baadhi ya watu walioshiriki mifano ya Ukumbusho hapo awali waliacha kula kwa sababu waligundua kwamba walikuwa na tumaini la kuishi duniani, si mbinguni.
10. “Kondoo wengine” leo wana wajibu na tumaini gani?
10 “Kondoo wengine” wenye imani katika fidia, waliojiweka wakfu kwa Mungu, na ambao wanaunga mkono “kundi dogo” la watiwa-mafuta katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme wamekuwa wakikusanywa hasa tangu mwaka wa 1935. (Luka 12:32) Kondoo hawa wengine wana tumaini la kuishi milele duniani, lakini wako sawa na mabaki ya warithi wa Ufalme katika mambo mengine yote. Kama wakazi wageni katika Israeli la kale ambao walimwabudu Yehova na kuitii Sheria, kondoo wengine leo hukubali wajibu wa Kikristo, kama vile kuhubiri habari njema pamoja na washiriki wa Israeli la kiroho. (Wagalatia 6:16) Hakuna mkazi yeyote mgeni angeweza kuwa mfalme au kuhani wa Israeli. Vivyo hivyo, hakuna mshiriki yeyote wa kondoo wengine anayeweza kutawala au kuwa kuhani katika Ufalme wa mbinguni.—Kumbukumbu la Torati 17:15.
11. Tarehe ambayo mtu alijiweka wakfu inawezaje kuonyesha iwapo anaweza kuwa mmoja wa watiwa-mafuta?
11 Katika miaka ya 1930, ilianza kuwa wazi kwamba kwa ujumla, jamii ya kimbingu ilikuwa imechaguliwa. Sasa, kondoo wengine wenye tumaini la kuishi duniani wamekuwa wakikusanywa kwa miaka 70 hivi. Mtiwa-mafuta akiasi, yaelekea sana kwamba mshiriki wa kondoo wengine ambaye amekuwa akimtumikia Mungu kwa uaminifu kwa miaka mingi, ndiye anayeweza kuitwa achukue nafasi ya yule aliyeasi kati ya wale 144,000.
-