Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kukusanya Vitu Vilivyo Mbinguni na Vitu Vilivyo Duniani
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
    • 10. Ni kwa njia gani wale wanaoshiriki kunywa divai ya Ukumbusho ‘hushiriki katika damu ya Kristo’?

      10 Paulo aliandika hivi kuhusu divai ambayo Wakristo watiwa-mafuta hushiriki kunywa wakati wa Ukumbusho: “Kikombe cha baraka ambacho tunabariki, je, hicho si kushiriki katika damu ya Kristo?” (1 Wakorintho 10:16) Ni kwa njia gani wale wanaoshiriki kunywa divai ‘hushiriki katika damu ya Kristo’? Bila shaka, hawashiriki kutoa dhabihu ya fidia, kwa kuwa wao wenyewe wanahitaji ukombozi. Kupitia imani yao katika nguvu za ukombozi za damu ya Kristo, dhambi zao husamehewa, nao wanatangazwa kuwa waadilifu kwa ajili ya uzima huko mbinguni. (Waroma 5:8, 9; Tito 3:4-7) Ni kupitia damu ya Kristo iliyomwagwa kwamba wale warithi-washirika wa Kristo 144,000 ‘wanatakaswa,’ wanawekwa kando, na kusafishwa kutokana na dhambi ili wawe “watakatifu.” (Waebrania 10:29; Danieli 7:18, 27; Waefeso 2:19) Naam, kupitia damu yake iliyomwagwa, Kristo ‘alimnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa, naye akawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.’—Ufunuo 5:9, 10.

      11. Watiwa-mafuta huonyesha nini kwa kunywa divai ya Ukumbusho?

      11 Yesu alipoanzisha Ukumbusho wa kifo chake, aliwapa mitume wake waaminifu kikombe cha divai na kusema: “Kinyweeni, ninyi nyote; kwa maana hii inamaanisha ‘damu yangu ya agano,’ ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi.” (Mathayo 26:27, 28) Kama vile damu ya ng’ombe-dume na mbuzi ilivyohalalisha agano la Sheria kati ya Mungu na taifa la Israeli, damu ya Yesu ilihalalisha agano jipya ambalo Yehova angefanya pamoja na taifa la Israeli wa kiroho, kuanzia siku ya Pentekoste 33 W.K. (Kutoka 24:5-8; Luka 22:20; Waebrania 9:14, 15) Kwa kunywa divai ambayo inafananisha ‘damu ya agano,’ watiwa-mafuta wanaonyesha kwamba wameingizwa katika agano jipya na kwamba wanapata faida zake.

      12. Watiwa-mafuta hubatizwaje katika kifo cha Kristo?

      12 Watiwa-mafuta wanakumbushwa jambo lingine. Yesu aliwaambia hivi wafuasi wake waaminifu: “Kikombe ninachokunywa mtakunywa, na ubatizo ninaobatizwa mtabatizwa.” (Marko 10:38, 39) Baadaye, mtume Paulo alisema kwamba Wakristo ‘wamebatizwa katika kifo cha Kristo.’ (Waroma 6:3) Watiwa-mafuta hudhabihu maisha yao. Kifo chao ni cha kidhabihu kwa sababu wanatupilia mbali tumaini lolote la kupata uzima wa milele duniani. Ubatizo wa Wakristo hao watiwa-mafuta katika kifo cha Kristo unamalizika wakati ambapo, baada ya kufa wakiwa waaminifu, wanafufuliwa wakiwa viumbe wa roho ili ‘watawale wakiwa wafalme’ pamoja na Kristo mbinguni.—2 Timotheo 2:10-12; Waroma 6:5; 1 Wakorintho 15:42-44, 50.

  • Kukusanya Vitu Vilivyo Mbinguni na Vitu Vilivyo Duniani
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
    • 14. Watiwa-mafuta wanaimarishwaje kiroho kwa kushiriki kula mkate na kunywa divai?

      14 Kutiwa muhuri kwa mwisho kwa idadi ndogo ya Wakristo walio na mwito wa kutawala pamoja na Kristo mbinguni kunakaribia kumalizika. Hadi mwisho wa maisha yao hapa duniani ambayo wanayadhabihu, watiwa-mafuta huimarishwa kiroho wanaposhiriki kula mkate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho. Wanahisi wameunganishwa pamoja na ndugu na dada zao waliotiwa mafuta, wakiwa washiriki wa mwili wa Kristo. Kushiriki kula mkate na kunywa divai huwakumbusha kwamba wana wajibu wa kuwa waaminifu hadi kifo.—2 Petro 1:10, 11.

  • Kukusanya Vitu Vilivyo Mbinguni na Vitu Vilivyo Duniani
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 15
    • [Sanduku katika ukurasa wa 23]

      “Mwili wa Kristo”

      Kwenye 1 Wakorintho 10:16, 17, Paulo alitumia neno “mwili” kwa njia ya pekee alipokuwa akizungumzia maana hususa ya mkate kwa ndugu za Kristo waliotiwa mafuta kwa roho. Alisema hivi: “Ule mkate ambao tunamega, je, huo si kushiriki katika mwili wa Kristo? Kwa sababu kuna mkate mmoja, sisi, ingawa tuko wengi, ni mwili mmoja, kwa maana sisi sote tunakula huo mkate mmoja.” Wakristo watiwa-mafuta wanaposhiriki kula mkate wa Ukumbusho, wanatangaza umoja wao katika kutaniko la watiwa-mafuta ambalo ni kama mwili, huku Kristo akiwa ndiye Kichwa.—Mathayo 23:10; 1 Wakorintho 12:12, 13, 18.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki