-
Kurudia Ili Kukazia MamboFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
UFUNDISHAJI bora hutia ndani kurudia mambo makuu. Jambo muhimu likitajwa zaidi ya mara moja, inaelekea wahudhuriaji watalikumbuka. Jambo hilo likirudiwa kwa njia tofauti kidogo, wanaweza kulielewa vizuri zaidi.
Ikiwa wasikilizaji hawatakumbuka mambo unayosema, maoni yao na maisha yao hayatabadilika. Labda wataendelea kufikiria mambo ambayo unakazia kwa njia ya pekee.
-
-
Kurudia Ili Kukazia MamboFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Katika Huduma ya Shambani. Unapohubiria watu, unatumaini kwamba watakumbuka mambo unayosema. Kurudia mambo makuu kwa njia nzuri kunaweza kuwakumbusha mambo hayo.
Kurudia jambo wakati linapozungumzwa hufanya libaki akilini. Basi, baada ya kusoma andiko, unaweza kulikazia kwa kuonyesha sehemu fulani ya andiko hilo na kuuliza, “Je, umeona maneno ambayo yametumiwa hapa?”
Pia unaweza kutumia vizuri maneno ya kumalizia mazungumzo. Kwa mfano, unaweza kusema: “Jambo kuu ambalo natumaini utakumbuka katika mazungumzo yetu ni . . . ” Kisha rudia kutaja jambo hilo kwa njia rahisi. Unaweza kusema hivi: “Kusudi la Mungu ni kuigeuza dunia kuwa paradiso. Kusudi hilo litatimizwa hakika.” Au labda: “Biblia inaonyesha wazi kwamba tunaishi katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo. Ili tusiangamizwe, ni lazima tujifunze matakwa ya Mungu.” Au tunaweza kusema: “Kama tulivyoona, Biblia ina mashauri mazuri yanayotusaidia kushughulikia matatizo ya familia.” Nyakati nyingine unaweza tu kurudia kunukuu andiko la Biblia ili alikumbuke. Ili ufaulu, unahitaji kufikiri kwanza.
-
-
Kurudia Ili Kukazia MamboFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Unapotoa Hotuba. Unapotoa hotuba jukwaani, lengo lako lisiwe tu kuzungumza. Unataka wasikilizaji waielewe, waikumbuke, na kuitumia maishani. Ili ufaulu, rudia mambo makuu kwa njia nzuri.
Lakini ukirudia kutaja mambo makuu kupita kiasi, wasikilizaji watachoka kukusikiliza. Chagua kwa makini mambo yanayopaswa kukaziwa kwa njia ya pekee. Mara nyingi hayo ni mambo makuu ya hotuba yako, lakini pia yanaweza kutia ndani mambo ambayo yatawafaidi sana wasikilizaji.
Ili urudie vizuri mambo makuu, kwanza unaweza kuyataja kwenye utangulizi. Yataje kwa sentensi fupi-fupi ambazo zinaonyesha kwa ujumla mambo ambayo utazungumzia, au kwa maswali, au kwa mifano mifupi inayoonyesha mambo mtakayozungumzia. Unaweza kutaja idadi ya mambo unayotaka kuzungumzia na kuyaorodhesha. Kisha fafanua kila moja ya mambo hayo katika hotuba yako. Unaweza kutia mkazo kwenye sehemu kuu ya hotuba kwa kutaja tena kila jambo kuu kabla ya kuzungumzia jingine. Au unaweza kutumia mfano unaoonyesha jinsi ya kutumia jambo hilo maishani. Pia unaweza kukazia mambo makuu kwa kutumia umalizio unaorudia kuyataja, au unaoonyesha tofauti iliyoko kati ya mambo hayo makuu na mambo mengine, au unaojibu maswali yaliyozushwa, au unaotaja kifupi suluhisho la mambo ambayo ulizungumzia.
-