-
Alikaa Macho, na AlingojaMnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
-
-
Nabii wa Yehova alianza kufuata barabara ambayo Ahabu alipitia. Ilikuwa safari ndefu katika giza na matope. Kisha jambo fulani la ajabu likatukia.
“Mkono wa Yehova ukawa juu ya Eliya, hivi kwamba akajifunga viuno, naye akakimbia mbele ya Ahabu mpaka Yezreeli.” (Mstari wa 46) Ni wazi kwamba “mkono wa Yehova” ulikuwa ukimwongoza Eliya kwa njia inayopita uwezo wa mwanadamu. Mji wa Yezreeli ulikuwa umbali wa kilomita 30 hivi, na Eliya hakuwa kijana.e Hebu wazia nabii huyo akiyafunga mavazi yake marefu kiunoni ili miguu yake isizuiliwe na chochote, kisha akikimbia katika barabara hiyo iliyojaa maji ya mvua kwa kasi sana hivi kwamba akafikia gari la farasi la mfalme, akalipita, na kuliacha!
Hiyo ilikuwa baraka kubwa kama nini kwa Eliya! Haikosi alisisimka sana kupata nguvu, afya, na uwezo huo ambao labda hata ulipita ule aliokuwa nao alipokuwa kijana. Huenda hilo likatukumbusha unabii unaowahakikishia watu waaminifu kwamba watapata afya kamilifu na nguvu katika Paradiso itakayokuwa duniani pote. (Isaya 35:6; Luka 23:43) Eliya alipokuwa akikimbia kwenye barabara yenye maji, bila shaka alijua kwamba alikuwa na kibali cha Baba yake, yule Mungu wa pekee wa kweli, Yehova!
-
-
Alikaa Macho, na AlingojaMnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 1
-
-
e Muda si muda, Yehova angempa Eliya kazi ya kumzoeza Elisha, ambaye angekuja kujulikana kuwa yule “aliyemimina maji juu ya mikono ya Eliya.” (2 Wafalme 3:11) Elisha alitumika akiwa mtumishi wa Eliya, kwa wazi akimsaidia nabii huyo mzee.
-