-
Kanuni za Adili Zinazostahili StahaMashahidi wa Yehova na Elimu
-
-
Haki ya Wazazi
Siku hizi, nchi zilizo nyingi hustahi haki ya wazazi ya kuwapa watoto wao maagizo ya kidini kwa kupatana na masadikisho yao. Dini zote huunga mkono haki hiyo, kama vile ionyeshwavyo na sheria iliyo halali bado katika Kanisa Katoliki: “Wakiwa wamewapa watoto wao uhai, wazazi wako chini ya ule wajibu imara wa kuwaelimisha, nao wana haki ya kufanya hivyo; hiyo ndiyo sababu ni lazima hasa waandalie watoto wao elimu ya Kikristo kulingana na fundisho la Kanisa.”—Sheria 226.
Watoto wanatiwa moyo wapendezwe na wengine
Mashahidi wa Yehova hawaombi jambo jingine zaidi. Wakiwa wazazi wenye kujali, wao hujaribu kukaza kikiki kanuni za Kikristo zilizo za kweli katika watoto wao na kukaza ndani yao upendo kwa jirani na staha kwa mali za watu wengine. Wao hutamani kufuata lile shauri ambalo mtume Paulo aliwapa Wakristo katika Efeso: “Wazazi, msiwatende watoto wenu kwa njia ya kuwakasirisha. Badala ya hivyo, waleeni kwa nidhamu na maagizo ya Kikristo.”—Waefeso 6:4, Today’s English Version.
-