-
Kitu Chenye Thamani Zaidi Kuliko Hazina za MisriMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
Aliporudishwa kwa binti Farao, Musa alifundishwa “katika hekima yote ya Wamisri.” (Matendo 7:22) Jambo hilo linadokeza kwamba Musa alizoezwa ili astahili kufanya kazi katika ofisi ya serikali. Elimu ya Misri ilitia ndani hesabu, usanifu majengo, ujenzi, sanaa, na sayansi. Huenda ikawa familia ya kifalme ilitaka Musa afundishwe dini ya Wamisri.
Huenda Musa alipata elimu yake ya pekee pamoja na wana wengine wa kifalme. Miongoni mwa watu walionufaika na elimu hiyo ya pekee ni “watoto wa watawala wa nchi za kigeni waliotumwa Misri au kupelekwa huko wakiwa mateka ili ‘kufanywa kuwa wastaarabu’ na baadaye kurudishwa wakatawale wakiwa vibaraka” waaminifu wa Farao. (The Reign of Thutmose IV, cha Betsy M. Bryan) Yaelekea nasari zilizojengwa kwenye majumba ya wafalme zilitayarisha vijana watumikie wakiwa maofisa kwenye nyumba ya mfalme.a Maandishi ya Ufalme wa Misri wa Kati (Nasaba ya 11 na 12) na Ufalme Mpya (Nasaba ya 18-20) yanaonyesha kwamba watumishi kadhaa wa Farao na maofisa wa ngazi za juu serikalini walidumisha jina hilo “Mtoto wa Nasari” hata walipokuwa watu wazima.
-
-
Kitu Chenye Thamani Zaidi Kuliko Hazina za MisriMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
a Huenda elimu hii ilikuwa sawa na elimu waliyopokea Danieli na wenzake ili kutumikia kwenye ofisi za serikali huko Babiloni. (Danieli 1:3-7) Linganisha na kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli!, sura ya 3, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.
-