Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kumbukumbu la Torati
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Septemba 15
    • “USISAHAU MAMBO AMBAYO MACHO YAKO YAMEONA”

      (Kumbukumbu la Torati 1:1–4:49)

      Katika hotuba ya kwanza, Musa anasimulia baadhi ya mambo yaliyotokea nyikani—hasa yale ambayo yatawasaidia Waisraeli wanapojitayarisha kuimiliki Nchi ya Ahadi. Lazima masimulizi kuhusu kuwekwa kwa waamuzi yawe yaliwakumbusha kwamba Yehova huwapanga watu wake katika njia inayohakikisha kwamba wanatunzwa kwa upendo. Musa pia anasimulia kwamba ile ripoti mbaya ya wapelelezi kumi ilifanya vizazi vilivyofuata visiingie katika nchi waliyoahidiwa. Wazia jinsi wasikilizaji wa Musa walivyoguswa moyo na mfano huo wa kuonya huku nchi waliyoahidiwa ikiwa mbele ya macho yao.

      Bila shaka, kukumbuka ushindi mbalimbali ambao Yehova aliwapa Waisraeli kabla ya kuvuka Yordani kuliwachochea wawe na ujasiri, kwa kuwa walikuwa tayari kuanza kuteka nchi iliyokuwa ng’ambo ya mto. Nchi ambayo walikuwa karibu kuimiliki ilijaa ibada ya sanamu. Ilifaa sana Musa awaonye kuhusu ibada hiyo.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kumbukumbu la Torati
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Septemba 15
    • MPENDE YEHOVA, NA KUTII AMRI ZAKE

      (Kumbukumbu la Torati 5:1–26:19)

      Katika hotuba yake ya pili, Musa anazungumzia kutolewa kwa Sheria kwenye Mlima Sinai, naye anazitaja tena zile Amri Kumi. Mataifa saba yametajwa waziwazi kwamba yataharibiwa kabisa. Wana wa Waisraeli wanakumbushwa jambo fulani muhimu walilojifunza nyikani: “Mwanadamu haishi kwa mkate tu bali mwanadamu huishi kwa kila neno la kinywa cha Yehova.” Katika hali yao mpya, lazima ‘washike amri yote.’—Kumbukumbu la Torati 8:3; 11:8.

      Wanapoingia katika nchi waliyoahidiwa, Waisraeli watahitaji sheria kuhusu ibada, hukumu, utawala, vita, na pia kuhusu maisha yao ya faraghani na ya kijamii. Musa anapitia sheria hizo na kukazia kwamba wanahitaji kumpenda Yehova na kutii sheria zake.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kumbukumbu la Torati
    Mnara wa Mlinzi—2004 | Septemba 15
    • Kabla ya Waisraeli kuvuka Mto Yordani na kuingia Kanaani, Musa anawatayarisha kwa ajili ya kazi kubwa iliyo mbele yao. Jinsi gani? Kwa kutoa mfululizo wa hotuba ambazo zinawatia moyo, kuwahimiza, na kuwaonya. Anawakumbusha Waisraeli kwamba wanapaswa kujitoa kikamili kwa Yehova Mungu, na kwamba hawapaswi kuiga mataifa yanayowazunguka. Hotuba hizo ndizo zinazofanyiza sehemu kubwa ya kitabu cha Kumbukumbu la Torati. Leo sisi tunahitaji mashauri yanayotolewa katika hotuba hizo, kwa kuwa sisi pia tunaishi katika ulimwengu ambapo si rahisi kujitoa kikamili kwa Yehova.—Waebrania 4:12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki