Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Kumbukeni Siku Zilizopita” kwa Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Lile himizo la bidii la “kumbuka siku za kale, [ku]tafakari miaka ya vizazi vingi” lilikuwa habari yenye kutokea tena na tena katika hotuba ambazo Musa aliwatolea Waisraeli, alipolisihi sana hilo taifa lionyeshe uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova bila hofu. (Kumbukumbu la Torati 32:7) Ona maneno yake, yaliyorekodiwa kwenye Kumbukumbu la Torati 7:18: “Usiwaogope [Wakanaani]; kumbuka sana BWANA, Mungu wako, alivyomfanya Farao na Misri yote.” Kule kukumbuka matendo yenye kuokoa ya Yehova kwa niaba ya watu wake kulipaswa kuwa kichocheo cha kuendelea kwao kushikamana kwa uaminifu na sheria za Mungu.—Kumbukumbu la Torati 5:15; 15:15.

  • “Kumbukeni Siku Zilizopita” kwa Nini?
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 1
    • Pili, kutosahau kwaweza kuwa njia ya kujifunza kutokana na makosa ya wakati uliopita na matokeo yayo. Akifikiria hilo, Musa alishauri Waisraeli hivi: “Kumbuka, usisahau ulivyomtia BWANA, Mungu wako, kasirani jangwani; tangu siku uliyotoka nchi ya Misri hata mlipofika mahali hapa, mmekuwa na uasi juu ya BWANA.” (Kumbukumbu la Torati 9:7) Kama Musa alivyoonyesha, tokeo la kutotii huko kwa Waisraeli lilikuwa kwamba ‘BWANA Mungu wao aliwaongoza miaka arobaini katika jangwa.’ Kwa nini walitiwa moyo kukumbuka hilo? Ilikuwa ili wanyenyekezwe na wasahihishe njia zao za uasi ili kwamba ‘wangezishika amri za BWANA, Mungu wao, wapate kwenda katika njia zake na kumcha.’ (Kumbukumbu la Torati 8:2-6) Walipaswa kujifunza katika maana ya kutorudia makosa yao ya wakati uliopita.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki