-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Kwa kufaa, hao mashahidi wawili wanaonwa sasa wakifanya ishara zinazokumbusha zile za Musa na Eliya. Mathalani, Yohana anasema hivi kwa habari yao: “Na ikiwa yeyote anataka kudhuru wao, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwala adui zao; na ikiwa yeyote angepaswa kutaka kudhuru wao, kwa jinsi hii yeye lazima auawe. Hawa wana mamlaka kufunga mbingu ili kwamba mvua isianguke wakati wa kutoa kwao unabii.”—Ufunuo 11:5, 6a, NW.
16. (a) Ishara inayohusu moto inatukumbushaje wakati ambao mamlaka ya Musa ilipokaidiwa katika Israeli? (b) Viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walikaidije Wanafunzi wa Biblia na wakachochea matata kwa ajili yao wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu, na hao walijipiganiaje?
16 Hii inatukumbusha wakati ambao mamlaka ya Musa ilipingwa katika Israeli. Nabii huyo alitamka maneno ya hukumu yenye moto, na Yehova aliwaharibu waasi hao, akila 250 kwa moto halisi kutoka mbinguni. (Hesabu 16:1-7, 28-35) Hali kadhalika, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo walikaidi Wanafunzi wa Biblia, wakisema kwamba hao hawakuwa wamehitimu kamwe katika makoleji ya kitheolojia. Lakini mashahidi wa Mungu walikuwa na vitambulisho vya juu zaidi vya kuwa wahudumu: wale watu wasikivu waliotii ujumbe wao wa Kimaandiko. (2 Wakorintho 3:2, 3) Katika 1917 Wanafunzi wa Biblia walitangaza The Finished Mystery, elezo lenye nguvu juu ya Ufunuo na Ezekieli. Hicho kilifuatwa na mgawanyo wa nakala 10,000,000 za trakti ya kurasa nne The Bible Students Monthly ikiwa na makala kuu yenye kichwa “Anguko la Babuloni—Sababu Lazima Jumuiya ya Wakristo Iteseke Sasa—Tokeo la Mwisho.” Katika United States, wale viongozi wa kidini waliokasirika walitumia kichaa cha vita kuwa udhuru wa kufanya kitabu hicho kipigwe marufuku. Katika nchi nyinginezo kitabu hicho kilikaguliwa kabla ya kuruhusiwa. Hata hivyo, watumishi wa Mungu walifuliza kupiga vita kwa matoleo yenye moto ya trakti yenye kurasa nne iliyokuwa na kichwa Kingdom News. Kadiri siku ya Bwana ilivyoendelea, vichapo vingine vilionyesha wazi hali ya kufa kiroho ya Jumuiya ya Wakristo.—Linga Yeremia 5:14.
-
-
Kuhuisha Mashahidi WawiliUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
18. (a) Ni mamlaka gani waliyopewa mashahidi wawili, na ni jinsi gani ni kama ile aliyopewa Musa? (b) Mashahidi wawili walifichuaje Jumuiya ya Wakristo?
18 Yohana anazidi kusema hivi juu ya wale mashahidi wawili: “Na wao wana mamlaka juu ya maji kuyageuza kuwa damu na kupiga dunia kwa kila aina ya tauni mara nyingi kadiri watakavyo.” (Ufunuo 11:6b, NW) Ili kumsadikisha Farao aruhusu Israeli waende wakiwa huru, Yehova alitumia Musa apige Misri yenye uonevu kwa tauni kutia na kugeuza maji kuwa damu. Karne nyingi baadaye, Wafilisti adui za Israeli walikumbuka vizuri matendo ya Yehova dhidi ya Misri, hiyo ikiwafanya walie: “Ni nani ataokoa sisi kutoka mkono wa Mungu huyu mwenye fahari ya kifalme? Huyu ndiye yule Mungu ambaye alikuwa mpigaji wa Misri kwa kila aina ya uchinjaji [“mapigo,” Union Version] katika nyika.” (1 Samueli 4:8 NW; Zaburi 105:29) Musa alifananisha Yesu, ambaye alikuwa na mamlaka kutamka hukumu za Mungu juu ya viongozi wa kidini wa siku yake. (Mathayo 23:13; 28:18; Matendo 3:22) Na wakati wa vita ya kwanza ya ulimwengu ndugu za Kristo, wale mashahidi wawili, walifichua ile hali ya “maji” yenye kuleta kifo ambayo Jumuiya ya Wakristo ilikuwa ikiwapa makundi yayo.
-