-
Hekalu Kubwa la Kiroho la YehovaMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 1
-
-
7. (a) Mungu alitia mafuta “Patakatifu pa Patakatifu” lini, na hilo lilimaanisha nini? (b) Ni nini kingine kilichompata Yesu wakati wa ubatizo wake?
7 Wakati wa ubatizo wa Yesu, makao ya kimbingu ya Mungu yalitiwa mafuta, au kutengwa, kuwa “Patakatifu pa Patakatifu” (NW) katika ule mpango wa hekalu kubwa la kiroho. (Danieli 9:24)
-
-
Hekalu Kubwa la Kiroho la YehovaMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 1
-
-
Patakatifu Zaidi Sana pa Kimbingu
8. Kiti cha ufalme cha Mungu mbinguni kilikuwa kimepata sehemu gani mpya sasa?
8 Katika siku ya ubatizo wa Yesu, kiti cha ufalme cha Mungu cha kimbingu kilikuwa kimepata sehemu mpya mbalimbali. Kuainishwa kwa dhabihu kamilifu ya kibinadamu ya kufunika dhambi za ulimwengu kulikazia utakatifu wa Mungu kwa kutofautishwa na hali yenye dhambi ya mwanadamu. Rehema ya Mungu pia ilikaziwa kwa njia ya kwamba sasa alionyesha kuwa kwake tayari kutulizwa, au kuridhishwa. Kwa njia hiyo kiti cha ufalme cha Mungu mbinguni kilikuwa kumekuwa sawa na chumba cha ndani cha hekalu, mahali ambapo kuhani wa cheo cha juu aliingia mara moja kwa mwaka akiwa na damu ya wanyama ili kufunika dhambi kwa njia ya kielezi.
9. (a) Pazia kati ya Patakatifu na Patakatifu Zaidi Sana lilifananisha nini? (b) Yesu aliingiaje ndani kupita lile pazia la hekalu la kiroho la Mungu?
9 Lile pazia lililotenganisha Patakatifu na Patakatifu Zaidi Sana lilifananisha mwili wa Yesu wenye nyama. (Waebrania 10:19, 20) Lilikuwa kizuizi kilichomzuia Yesu asiingie mbele ya Babaye alipokuwa mwanadamu duniani. (1 Wakorintho 15:50) Wakati wa kifo cha Yesu, ‘pazia la hekalu lilipasuka vipande viwili toka juu hata chini.’ (Mathayo 27:51) Hilo lilionyesha kwa njia yenye kutokeza kwamba kizuizi kilichomzuia Yesu asiingie mbinguni sasa kilikuwa kimeondolewa. Siku tatu baadaye, Yehova Mungu alifanya muujiza wenye kutokeza. Alimfufua Yesu kutoka kwa wafu, si akiwa mwanadamu awezaye kufa mwenye nyama na damu, bali akiwa kiumbe kitukufu cha kiroho, ‘akaaye milele.’ (Waebrania 7:24) Siku arobaini baadaye, Yesu alipaa kwenda mbinguni akaingia “Patakatifu pa Patakatifu” (NW) palipo halisi, “aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu.”—Waebrania 9:24.
10. (a) Ni nini kilichotendeka baada ya Yesu kumtolea Babaye wa kimbingu thamani ya dhabihu yake? (b) Kutiwa mafuta kwa roho takatifu kulimaanisha nini kwa wanafunzi wa Kristo?
10 Je, Mungu alikubali thamani ya damu ya Yesu iliyomwagwa kuwa ufuniko kwa ajili ya dhambi za ulimwengu? Kwa kweli aliikubali. Ithibati ya kukubali huko ilikuja siku 50 kamili baada ya ufufuo wa Yesu, kwenye siku ya msherehekeo wa Pentekoste. Roho takatifu ya Mungu ilimwagwa juu ya wanafunzi wa Yesu 120 waliokusanyika pamoja katika Yerusalemu. (Matendo 2:1, 4, 33) Sawa na Kuhani wao wa Cheo cha Juu, Yesu Kristo, sasa walikuwa wametiwa mafuta ili watumikie wakiwa ‘ukuhani mtakatifu, watoe dhabihu za roho’ chini ya mpango wa Mungu wa hekalu kubwa la kiroho. (1 Petro 2:5) Zaidi ya hayo, hawa watiwa-mafuta walifanyiza taifa jipya, “taifa takatifu” la Mungu la Israeli wa kiroho. Kuanzia wakati huo na kuendelea, unabii wote mbalimbali wa mambo mazuri juu ya Israeli, kama ile ahadi ya “agano jipya” iliyorekodiwa kwenye Yeremia 31:31, ungehusu kutaniko la Kikristo la watiwa-mafuta, “Israeli wa Mungu” walio halisi.—1 Petro 2:9; Wagalatia 6:16.
-