-
Yale Anayotabiri Yehova YanatimiaMnara wa Mlinzi—2008 | Januari 1
-
-
Mataifa ya Kale
Mungu alitabiri kwamba Babiloni lingeharibiwa milele na kwamba mataifa ya Edomu, Moabu, na Amoni pia yangeharibiwa milele. (Yeremia 48:42; 49:17, 18; 51:24-26; Obadia 8, 18; Sefania 2:8, 9) Kutoweka kwa mataifa hayo kunathibitisha usahihi wa Neno la Mungu la kinabii.
Bila shaka, huenda mtu akabisha kwamba mtu yeyote anaweza kutabiri kuwa taifa fulani, hata likiwa na nguvu kadiri gani, litatoweka. Lakini hoja hiyo inapuuza uhakika ulio muhimu kwamba Biblia ilitoa habari zaidi. Kwa mfano, ilitoa habari zaidi kuhusu namna jiji la Babiloni lingeangushwa. Biblia ilitabiri kwamba jiji hilo lingeharibiwa na Wamedi, kwamba askari-jeshi wavamizi wangekuwa chini ya uongozi wa Koreshi, na kwamba mito iliyozunguka jiji hilo na kulipa ulinzi ingekauka.—Isaya 13:17-19; 44:27–45:1.
Biblia haikutabiri kwamba watu au mataifa yote yaliyoshindwa yangetoweka milele. Kinyume na hilo, akitabiri kuhusu kuharibiwa kwa Yerusalemu na Wababiloni, Mungu alisema kwamba wakaaji wa jiji hilo wangerudishwa, ingawa Wababiloni hawakuwa na zoea la kuwaachilia huru mateka wao. (Yeremia 24:4-7; 29:10; 30:18, 19) Hilo lilitimia, na wazao wa Wayahudi wanaendelea kuishi wakiwa taifa mpaka leo.
Zaidi ya hayo, Yehova alitabiri kwamba Misri ambayo ilikuwa serikali kuu ya ulimwengu ingepinduliwa lakini ‘baadaye watu wangekaa ndani yake kama katika siku za zamani za kale.’ Baada ya muda, serikali hiyo ya kale ‘ingekuwa ufalme wa hali ya chini.’ (Yeremia 46:25, 26; Ezekieli 29:14, 15) Hilo pia lilitimia. Zaidi ya hilo, Yehova alitabiri kwamba serikali ya Ugiriki ambayo pia ilikuwa serikali kuu ya ulimwengu ingepinduliwa, lakini hakusema kamwe kwamba taifa hilo lingetoweka. Tunajifunza nini kuhusu kutoweka kwa mataifa ambayo Yehova alitabiri kwamba yangetoweka na kuendelea kuwapo kwa mataifa ambayo hakutabiri kuwa yangetoweka? Kwamba Neno la Mungu lina unabii wa kweli na wenye kutegemeka.
-
-
Yale Anayotabiri Yehova YanatimiaMnara wa Mlinzi—2008 | Januari 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 22, 23]
Neno la Mungu lilitabiri kutoweka kabisa kwa mataifa haya . . .
EDOMU
BABILONI
. . . lakini si kutoweka kwa
UGIRIKI
MISRI
[Hisani]
Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.
WHO photo by Edouard Boubat
-