-
“Bwana, Tufundishe Jinsi ya Kusali”Mnara wa Mlinzi—2004 | Februari 1
-
-
Unabii wa Danieli unafananisha Ufalme wa Kimasihi na “jiwe” lililokatwa kutoka ‘mlimani.’ (Danieli 2:34, 35, 44, 45) Mlima unafananisha enzi kuu ya Yehova, kwa hiyo Ufalme unaofananishwa na jiwe ni wonyesho mpya wa utawala wa Yehova juu ya ulimwengu. Katika unabii huo, jiwe nalo ‘linakuwa mlima mkubwa na kuijaza dunia yote,’ kuonyesha kwamba Ufalme wa Kimasihi utawakilisha mamlaka kuu ya Mungu katika kutawala dunia.
-
-
“Bwana, Tufundishe Jinsi ya Kusali”Mnara wa Mlinzi—2004 | Februari 1
-
-
Kwa hiyo, je, bado inafaa tusali Ufalme huo “uje”? Bila shaka. Kwa kuwa katika unabii wa Danieli, Ufalme wa Kimasihi unaofananishwa na jiwe, utaponda serikali za kisiasa za wanadamu, zinazofananishwa na sanamu kubwa. Jiwe hilo litaiponda-ponda sanamu hiyo iwe kama unga. Unabii wa Danieli unasema: “Ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”—Danieli 2:44.
-