Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
    • HAKUNA SERIKALI NYINGINE KUU YA ULIMWENGU ITAKAYOTOKEA

      13. Tunajua nini kuhusu sehemu ya tano ya sanamu ambayo Danieli anafafanua?

      13 Unabii mmoja katika kitabu cha Danieli unatuwezesha kujua tuko wapi katika mkondo wa wakati. Danieli anafafanua sanamu ya umbo la kibinadamu ambayo inafanyizwa kutokana na madini mbalimbali. (Dan. 2:​28, 31-33) Sanamu hiyo inafananisha mfuatano wa serikali kuu za ulimwengu ambazo zilikuwa na uvutano mkubwa juu ya watu wa Mungu, zamani na sasa. Serikali hizo ni Babiloni, Umedi na Uajemi, Ugiriki, Roma, na serikali kuu ya mwisho ambayo inatawala sasa. Uchunguzi wa unabii wa Danieli unaonyesha kwamba serikali hii kuu ya mwisho ya ulimwengu inafananishwa na miguu na vidole vya sanamu hiyo. Wakati wa Vita vya Kwanza vya Ulimwengu, Uingereza na Marekani zilianzisha ushirikiano wa pekee. Naam, sehemu ya tano ya sanamu ya Danieli ni Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani. Miguu ndiyo sehemu ya mwisho ya sanamu hiyo, na hilo linaonyesha kwamba hakuna serikali nyingine kuu ya kibinadamu itakayotokea baada ya serikali hiyo. Miguu na vidole vimefanyizwa kwa chuma na udongo, kuonyesha kwamba Muungano wa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani umedhoofika.

      14. Ni serikali gani kuu ya ulimwengu itakayokuwa ikitawala vita vya ­Har–​Magedoni vitakapoanza?

      14 Unabii huohuo unaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu, unaofananishwa na jiwe kubwa, ulikatwa kutoka kwenye mlima wa enzi kuu ya Yehova katika mwaka wa 1914. Jiwe hilo sasa linasonga kwa kasi sana ili kugonga shabaha yake, yaani, miguu ya sanamu hiyo. Katika vita vya ­Har–​Magedoni, miguu na sehemu nyingine za sanamu hiyo zitapondwa kabisa. (Soma Danieli 2:​44, 45.) Kwa hiyo, Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani bado itakuwa serikali kuu wakati vita vya ­Har–​Magedoni vitakapoanza. Itasisimua kama nini kuona unabii huo ukitimizwa kikamili!c Hata hivyo, Yehova atamchukulia Shetani hatua gani?

  • Jinsi Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Septemba 15
    • c Maneno “kuzikomesha falme hizi zote” yaliyo katika Danieli 2:44 yanarejelea falme, au serikali kuu za ulimwengu, zinazofananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu hiyo. Hata hivyo, unabii mwingine wa Biblia kama huo unaonyesha kwamba “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” watajipanga dhidi ya Yehova katika “siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu. 16:14; 19:​19-21) Kwa hiyo, si falme zinazofananishwa na sanamu hiyo tu zitakazoharibiwa kwenye ­Har–​Magedoni bali pia falme nyingine zote za ulimwengu huu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki