Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nehemia
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
    • Mambo Tunayojifunza:

      1:4; 2:4; 4:4, 5. Tunapokabili hali ngumu au tunapofanya maamuzi mazito, tunapaswa ‘kudumu katika sala’ na kutenda kulingana na mwongozo unaopatikana katika Neno la Mungu.—Waroma 12:12.

      1:11–2:8; 4:4, 5, 15, 16; 6:16. Yehova hujibu sala za watumishi wake zinazotolewa kwa unyoofu.—Zaburi 86:6, 7.

      1:4; 4:19, 20; 6:3, 15. Ingawa Nehemia alikuwa mtu mwenye huruma, aliweka mfano mzuri akiwa mtu mwenye bidii ambaye alitetea uadilifu kwa uthabiti.

      1:11–2:3. Shangwe ya Nehemia haikutokana na cheo chake chenye kuheshimika cha kuwa mnyweshaji. Ilitokana na kuendeleza ibada ya kweli. Ibada ya Yehova na mambo yote yanayoiunga mkono ndiyo yanayopaswa kuwa hangaiko letu kuu na chanzo kikuu cha shangwe yetu.

      2:4-8. Yehova alimchochea Artashasta amruhusu Nehemia kwenda kujenga upya ukuta wa Yerusalemu. Andiko la Methali 21:1 linasema hivi: “Moyo wa mfalme ni kama vijito vya maji mkononi mwa Yehova. Huugeuza kuelekea popote anapopenda.”

      3:5, 27. Hatupaswi kuona kazi ya mkono inayofanywa kwa kusudi la kuendeleza ibada ya kweli kuwa yenye kutushushia heshima, kama walivyofanya “watu wa [Watekoa] walio mashuhuri.” Badala yake, tunaweza kuwaiga Watekoa wa kawaida waliojitolea kwa hiari.

      3:10, 23, 28-30. Ingawa wengine wanaweza kuhamia maeneo yenye uhitaji wa wahubiri wa Ufalme, wengi wetu tunaunga mkono ibada safi mahali tunapoishi. Tunaweza kufanya hivyo kwa kushiriki kazi ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme na kusaidia waliokumbwa na misiba, lakini tunafanya hivyo zaidi kwa kuhubiri habari njema ya Ufalme.

      4:14. Tunapokabili upinzani, sisi pia tunaweza kushinda woga kwa kumkumbuka “Yeye ambaye ni mkuu na Mwenye kuogopesha.”

      5:14-19. Gavana Nehemia amewawekea waangalizi Wakristo mfano bora wa unyenyekevu, kutokuwa na ubinafsi, na busara. Ingawa alikuwa na bidii katika kutekeleza Sheria ya Mungu, hakuwanyanyasa wengine ili ajifaidi. Badala yake, aliwahangaikia walioteseka na maskini. Nehemia aliwawekea watumishi wote wa Mungu mfano mzuri wa ukarimu.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nehemia
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
    • Mambo Tunayojifunza:

      8:8. Tukiwa walimu wa Neno la Mungu, ‘tunaeleza maana yake’ kwa kuongea kwa njia inayosikika wazi, kukazia maneno, kufafanua Maandiko kwa usahihi, na kuonyesha matumizi yake vizuri.

      8:10. Tunapata “shangwe ya Yehova” kwa kujua na kutosheleza mahitaji yetu ya kiroho na kufuata mwongozo wa kitheokrasi. Tunapaswa kujifunza Biblia kwa bidii, kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida, na kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi kwa bidii!

      11:2. Kuacha urithi na kuhamia Yerusalemu kulitia ndani gharama na matatizo mbalimbali. Wale waliojitolea kuhama walionyesha roho ya kujidhabihu. Sisi pia tunaweza kuonyesha roho hiyohiyo kunapokuwa na uhitaji wa kujitolea kuwasaidia wengine makusanyikoni au katika pindi nyinginezo.

      12:31, 38, 40-42. Kuimba ni njia moja ya kumsifu Yehova na kumshukuru. Tunapokuwa kwenye mikutano ya Kikristo, tunapaswa kuimba kutoka moyoni.

      13:4-31. Tunapaswa kuwa macho tusiruhusu upendo wa mali, ufisadi, na uasi-imani utuathiri.

      13:22. Nehemia alitambua kwamba alikuwa na wajibu kwa Mungu. Sisi pia tunapaswa kutambua wajibu wetu kwa Yehova.

      Ni Muhimu Kuwa na Baraka za Yehova!

      Mtunga-zaburi aliimba hivi: “Yehova mwenyewe asipoijenga nyumba, ni bure kwamba wajenzi wake wameifanyia kazi ngumu.” (Zaburi 127:1) Kitabu cha Nehemia kinaonyesha vizuri sana ukweli wa maneno hayo!

      Jambo tunalojifunza liko wazi. Ikiwa tunataka kufanikiwa katika jambo lolote tunalofanya, ni lazima tupate baraka za Yehova. Je, tunaweza kutazamia baraka za Yehova ikiwa hatutangulizi ibada ya kweli maishani mwetu? Basi, kama Nehemia, acheni jambo kuu maishani mwetu liwe kuendeleza ibada ya Yehova.

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nehemia
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Februari 1
    • Kitabu hicho kiliandikwa na Gavana Nehemia, na kinasimulia jinsi ibada ya kweli inavyokwezwa watu wanapochukua hatua thabiti na wanapomtegemea kabisa Yehova Mungu. Kinaonyesha waziwazi jinsi Yehova anavyoongoza mambo ili kutimiza mapenzi yake. Pia, kinasimulia kuhusu kiongozi mwenye nguvu na aliye jasiri. Ujumbe wa kitabu cha Nehemia una mambo muhimu kwa waabudu wote wa kweli leo, “kwa maana neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu.”—Waebrania 4:12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki