-
“Bila Kielezi Hakuwa Akisema Nao”Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
-
-
14. Katika mfano wa Msamaria mwema, kwa nini Yesu alitumia barabara ‘iliyotoka Yerusalemu kwenda Yeriko’ kukazia hoja yake?
14 Pili, kumbuka mfano wa Msamaria mwema. Yesu alianza kwa kusema: “Mtu fulani alikuwa akiteremka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko akaanguka miongoni mwa wapokonyaji, ambao walimvua nguo na pia kumpiga, wakaenda zao, wakimwacha yeye nusura kufa.” (Luka 10:30) Yesu alitumia barabara ‘iliyotoka Yerusalemu kwenda Yeriko’ kukazia hoja yake. Yesu alisimulia mfano huo akiwa Yudea, karibu na Yerusalemu; kwa hiyo yaelekea wasikilizaji wake walijua barabara hiyo. Barabara hiyo ilikuwa hatari sana hasa kwa mtu aliyetembea peke yake. Ilijipinda-pinda kwa hiyo kulikuwa na sehemu nyingi ambazo wahalifu wangeweza kuotea.
15. Kwa nini hakuna mtu ambaye angeweza kutetea kutojali kwa kuhani na Mlawi katika kielezi cha Msamaria mwema?
15 Pia tunapaswa kutambua jambo jingine ambalo Yesu alitaja kuhusu barabara “kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko.” Kulingana na simulizi hilo, kuhani ndiye aliyekuwa wa kwanza kupita katika barabara hiyo kisha akafuatwa na Mlawi, lakini wote wawili hawakusimama kumsaidia mtu huyo. (Luka 10:31, 32) Makuhani walitumikia hekaluni huko Yerusalemu, na walisaidiwa na Walawi. Makuhani na Walawi wengi walikaa Yeriko wakati ambapo hawakuwa wakifanya kazi hekaluni, kwa kuwa Yeriko lilikuwa umbali wa kilometa 23 tu kutoka Yerusalemu. Kwa hiyo, bila shaka walipita katika barabara hiyo mara kwa mara. Pia, ona kwamba kuhani na Mlawi walikuwa wakitembea katika barabara ‘iliyotoka Yerusalemu,’ hivyo wakielekea mbali na hekalu.b Kwa hiyo hakuna mtu ambaye angeweza kutetea kutojali kwa watu hao kwa kusema, ‘Walikwepa mtu huyo aliyejeruhiwa kwa sababu alionekana ni kama amekufa, na kugusa maiti kungefanya wasitumikie hekaluni.’ (Mambo ya Walawi 21:1; Hesabu 19:11, 16)
-
-
“Bila Kielezi Hakuwa Akisema Nao”Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
-
-
b Yerusalemu lilikuwa katika nyanda za juu kuliko Yeriko. Kwa hiyo kama ilivyotajwa katika mfano huo, msafiri angekuwa “akiteremka” anaposafiri “kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko.”
-