-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kuvumisha Kichocheo cha “Kusonga Mbele”
Ujapokuwa upimiwaji vyakula na petroli katika wakati wa vita, mapema katika Machi 1942, mipango ilitangazwa ya Ulimwengu Mpya Kusanyiko la Kitheokrasi, ambalo lingefanywa Septemba 18-20. Ili kurahisisha usafiri, majiji 52 ya mkusanyiko yaliteuliwa kote Marekani, mengi kati yayo yakiunganishwa kwa waya za simu na Cleveland, Ohio, jiji kuu. Karibu na wakati huohuo, Mashahidi wa Yehova walikusanyika katika majiji mengine 33 kotekote duniani. Ni nini lililokuwa lengo la kusanyiko hilo?
‘Sisi hatukukusanyika hapa ili kutafakari juu ya wakati uliopita au yale yaliyofanywa na watu mmoja-mmoja,’ akataarifu mwenyekiti, Ndugu Covington, katika maneno yake ya utangulizi kwa ajili ya kipindi cha kufungua. Kisha, akatoa utangulizi kwa hotuba ya msingi, “Ile Nuru Pekee,” ikitegemea Isaya sura 59 na 60, iliyotolewa na Ndugu Franz. Akirejezea amri ya kiunabii ya Yehova iliyoandikwa na Isaya, msemaji alijulisha hivi kwa kuchochea: “Hapa, basi, kipo kichocheo cha ‘Kusonga mbele’ kutoka kwa Mamlaka Iliyo Juu Zaidi ili kufuliza kuendelea na [kazi] yake ya kutoa ushahidi hata iweje kabla ya Har–Magedoni kuja.” (Isa. 6:1-12) Haukuwa wakati wa kulegeza mkono na kustarehe.
“Kuna kazi zaidi ya kufanywa; kazi nyingi!” akajulisha N. H. Knorr katika hotuba iliyofuata katika programu. Ili kusaidia wasikilizaji wake katika itikio lao kwa kichocheo cha “Kusonga mbele,” Ndugu Knorr alitangaza kutolewa kwa chapa ya tafsiri ya Biblia ya King James, iliyochapwa kwenye matbaa za Sosaiti yenyewe na ikiwa kamili pamoja na konkodansi iliyokusudiwa hasa kwa matumizi ya Mashahidi wa Yehova katika huduma yao ya shambani. Kitolewaji hicho kilionyesha kupendezwa sana kwa Ndugu Knorr katika uchapaji na ugawanyaji wa Biblia. Kwa kweli, baada ya yeye kuwa msimamizi wa Sosaiti mapema mwaka huo, Ndugu Knorr alikuwa amechukua hatua ya haraka kupata haki ya uchapaji ya tafsiri hiyo na kuratibu utayarishaji wa konkodansi na mambo mengine. Katika muda wa miezi michache chapa hiyo ya pekee ya King James Version ilikuwa tayari kutolewa kwenye kusanyiko.
Katika siku ya mwisho ya kusanyiko, Ndugu Knorr alitoa hotuba “Amani—Je, Inaweza Kudumu?” Katika hotuba hiyo yeye alionyesha uthibitisho wenye nguvu kutoka Ufunuo 17:8 kwamba Vita ya Ulimwengu 2, iliyokuwa ikichacha wakati huo, haingeendelea kufikia Har–Magedoni, kama vile wengine walivyofikiri, bali kwamba vita hiyo ingekoma na kipindi cha amani kingekuja. Kulikuwa kungali kuna kazi ya kufanywa katika kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu. Wakusanyikaji waliambiwa kwamba ili kusaidia kuangalia ukuzi uliotazamiwa katika tengenezo, kuanzia mwezi uliofuata Sosaiti ingepeleka “watumishi wa akina ndugu” kufanya kazi pamoja na makutaniko. Kila kutaniko lingetembelewa kila miezi sita.
“Ulimwengu Mpya Kusanyiko la Kitheokrasi liliunganisha tengenezo la Yehova pamoja kwa imara kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele,” asema Marie Gibbard, aliyehudhuria katika Dallas, Texas, pamoja na wazazi wake. Na kulikuwa na kazi nyingi ya kufanywa. Mashahidi wa Yehova walitazama mbele kwenye kipindi cha amani kilichokuwa kikija. Walikuwa wameazimia kuzidi kusonga mbele kupitia upinzani na mnyanyaso, wakijulisha habari njema bila kuacha!
-
-
Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 93]
Kitia-Moyo cha Kutazama Mbele
Wajumbe kwenye Ulimwengu Mpya Kusanyiko la Kitheokrasi katika Cleveland, Ohio, katika Septemba 1942, walifurahi wakati mwandishi-mweka-hazina wa Sosaiti aliye mzee-mzee, W. E. Van Amburgh, alipohutubia kusanyiko. Ndugu Van Amburgh alikumbuka kwamba mkusanyiko wa kwanza aliohudhuria ulikuwa katika Chicago katika 1900, na ulikuwa mkusanyiko “mkubwa”—walikuwa kama 250 waliohudhuria. Baada ya kutaja mikusanyiko mingine “mikubwa” katika muda wa miaka iliyopita, alimalizia kwa kitia-moyo hiki cha kutazama mbele: “Mkusanyikok huu waonekana kuwa mkubwa kwetu sasa, lakini kama vile mkusanyiko huu ulivyo mkubwa zaidi kwa kulinganishwa na ile ambayo nimehudhuria katika miaka iliyopita, ndivyo ninavyotarajia kwamba mkusanyiko huu utakuwa mdogo sana ukilinganishwa na ile ya wakati ujao wa karibu wakati Bwana aanzapo kukusanya watu wake kutoka kona zote za dunia.”
[Maelezo ya Chini]
k Kilele cha watu 26,000 walihudhuria katika Cleveland, kukiwa jumla ya hudhurio ya watu 129,699 ya yale majiji 52 ya mkusanyiko yaliyotapakaa kotekote Marekani.
-