-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
New Zealand: Wakati wa mapumziko ya mchana, dada kijana anayeitwa Cecilia alikuwa akisoma broshua fulani inayozungumzia Biblia. Mfanyakazi mwenzake alimuuliza kuihusu. Cecilia alipokuwa akieleza kuhusu yaliyomo katika broshua hiyo, watu 15 walikusanyika ili kumsikiliza, akiwemo mkubwa wake aliyemwalika ofisini mwake baadaye. Alimwambia Cecilia kwamba alivutiwa na yale aliyokuwa amesikia. Pia aliwaeleza wafanyakazi kwamba chumba cha kulia chakula cha mchana kingetumiwa kwa ajili ya majadiliano ya Biblia. Vilevile alirefusha muda wa mapumziko wa Cecilia kwa dakika 30 ili awe na nafasi ya kula na pia ya kuzungumzia Biblia. Kwa majuma manne, watu 9 hadi 15 walijiunga na majadiliano hayo. Wanawake wawili hujifunza Biblia kwa ukawaida sasa, wanafanya maendeleo kwa haraka, na wanawahubiria watu wa familia zao na marafiki wao.
-
-
Ripoti ya Ulimwenguni Pote2006 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 57]
Cecilia, New Zealand
-