-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Walijitoa Wenyewe kwa Hiari
Makolpota hao walikuwa watanguliza-njia kwelikweli. Waliingia hadi kwenye sehemu za nchi zisizoweza kufikika katika wakati ambapo usafiri ulikuwa wa nyuma sana na sehemu kubwa ya barabara ilikuwa vijia tu vya mikokoteni. Dada Early, katika New Zealand, ni mmoja wa wale waliofanya hivyo. Akianza mapema kabla ya Vita ya Ulimwengu 1, alitumia miaka 34 katika utumishi huo wa wakati wote kabla hajafa katika 1943. Alienda sehemu nyingi za nchi hiyo kwa baiskeli. Hata alipolemaa kwa ugonjwa wa yabisi kavu na hivyo hangeweza kuiendesha, alitumia baiskeli ili aiegemee na kubebea vitabu vyake katika eneo la kibiashara la Christchurch. Yeye angeweza kupanda ngazi, lakini alilazimika kuzishuka kwa kwenda kinyumenyume kwa sababu ya udhaifu wake wenye kulemaza. Hata hivyo maadamu alikuwa na nguvu kidogo, aliitumia katika utumishi wa Yehova.
-
-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 284]
Dada Early alisafiri sehemu kubwa ya New Zealand kwa baiskeli ili kushiriki ujumbe wa Ufalme
-