-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Nikaragua
Katika mwaka wa 2006 ndugu walifaulu kwa mara ya kwanza kuwahubiria kikamili watu wa kabila la Mayangna. Watu wengi wa kabila hilo ni waumini wa Kanisa la Moravia. Hilo ni kanisa la Kiprotestanti, na katika miji mingi kasisi wa kanisa hilo anatumika kama meya ijapokuwa hajawekwa rasmi. Mmoja wa makasisi hao alivunja desturi na kuwaruhusu mapainia Hamilton na Abner kukaa mjini mwake. Hata aliwatafutia makao na akawapa Biblia kamili katika lugha ya Mayangna. Ndugu hao walijifunza lugha hiyo na muda si muda walikuwa na mafunzo kadhaa ya Biblia. Hata waliweza kutafsiri hotuba katika ziara ya kwanza ya mwangalizi wa mzunguko wakati watu 13 walipohudhuria mkutano, na pia wakati watu 90 walipohudhuria Ukumbusho. Ndugu hao walitafsiri pia nyimbo mbili zilizoteuliwa kwa ajili ya Ukumbusho, na wote waliimba kwa shangwe.
Kwa sababu watu wengi wanapendezwa, ofisi ya tawi ilikubali ndugu hao wabaki katika eneo hilo. Lakini, je, wenye mamlaka walikubali? Katika mkutano wa baraza la mji, watu fulani waliwashtaki Mashahidi wa Yehova kwamba wao ni mpinga-Kristo. Hata hivyo, mtu mmoja aliyekuwa amejifunza na Mashahidi, na ambaye ni mwanachama wa baraza hilo, alisema: “Tangu vijana hao walipofika mjini kwetu, sijawahi kumwona mtu yeyote akiwapikia wala kuwafulia nguo. Wanajishughulikia wenyewe. Hata wamejifunza lugha yetu! Isitoshe, wametufundisha mambo ya Biblia ambayo hatukujua. Ikiwa watu hao hawangekuwa wametumwa na Mungu, hakika wangekuwa tayari wamechoka.” Ndugu hao waliruhusiwa kubaki huko.
-
-
Matukio Muhimu ya mwaka uliopita2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 21]
Hamilton na Abner wakifundisha Biblia katika lugha ya Mayangna
-