Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Babeli Umeanguka”!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 20. Kwa nini ufunuo uliorekodiwa kwenye Isaya 21:11, 12 ni muhimu kwa watu wa Yehova leo?

      20 Ufunuo huo mfupi umemaanisha mambo mengi kwa watu wa Yehova leo.e Twajua kuwa wanadamu wako ndani sana ya usiku wenye giza la upofu wa kiroho na kutengwa kutoka kwa Mungu ambao utaongoza kwenye kuharibiwa kwa mfumo huu wa mambo. (Waroma 13:12; 2 Wakorintho 4:4) Wakati huu wa usiku, nuru yoyote ile ya kutumaini eti huenda kwa njia fulani mwanadamu akaleta amani na usalama ni kama ile nuru ya mapambazuko yenye kudanganya ambayo hufuatwa tu na nyakati zenye giza hata zaidi. Mapambazuko ya kweli yanakaribia—mapambazuko ya Utawala wa Mileani wa Kristo juu ya dunia hii. Lakini maadamu usiku upo, ni sharti tufuate mwongozo wa jamii ya mlinzi kwa kudumu tukiwa macho kiroho na kutangaza kwa moyo mkuu kukaribia kwa mwisho wa mfumo huu wa mambo wenye ufisadi.—1 Wathesalonike 5:6.

  • “Babeli Umeanguka”!
    Unabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 18. Ufunuo unaosema, “Mchana unakuja na usiku pia,” watimizwaje juu ya Edomu ya kale?

      18 Wakati wa kuandikwa kwa kitabu cha Isaya, Edomu iko kwenye njia ya jeshi la Ashuru lenye nguvu. Baadhi ya watu huko Edomu wana hamu ya kujua wakati ambapo usiku wa kuonewa kwao utaisha. Kuna jibu gani? “Mlinzi akasema, Mchana unakuja na usiku pia.” (Isaya 21:12a) Mambo si mema kwa Edomu. Nuru hafifu ya asubuhi itachomoza kwenye upeo wa macho, lakini itakuwa ya muda mfupi, yenye kudanganya. Usiku—wakati mwingine wenye giza la uonezi—utafuatia upesi baada ya asubuhi. Hilo lawakilisha ipasavyo kama nini wakati ujao wa Edomu! Ukandamizaji wa Ashuru utaisha, lakini Babiloni itafuatia Ashuru ikiwa serikali ya ulimwengu nayo itaharibu Edomu. (Yeremia 25:17, 21; 27:2-8) Mambo hayo yatarudiwa. Ukandamizaji kutoka kwa Babiloni utafuatwa na ukandamizaji kutoka kwa Uajemi kisha kwa Ugiriki. Kisha kutakuwepo “asubuhi” fupi katika nyakati za Roma, wakati akina Herode—wenye asili ya Edomu—watakapochukua mamlaka huko Yerusalemu. Ingawa “asubuhi” hiyo haitadumu. Hatimaye, Edomu atashuka kwenye kimya cha kudumu, atokomee kabisa kutoka katika historia. Mwishowe jina Duma litamfaa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki