-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka uliofuata, Ingebret Andersen, ambaye aliishi karibu na jiji la Skien, alipata kitabu The Plan of the Ages, ambacho huenda kilikuwa mojawapo ya nakala ambazo Knud alileta Norway. Kwa muda mrefu, Ingebret alipendezwa na habari kuhusu kuja kwa Kristo kwa “mara ya pili,” na sasa yeye na mke wake Berthe, walivutiwa na mambo waliyosoma. Punde si punde, Ingebret akaanza kuhubiri. Hata alienda kwenye mikutano ya kidini ili kuwaambia watu kuhusu Utawala wa Miaka Elfu wa Kristo. Baadaye, aliwatembelea watu waliopendezwa, na muda si muda kukawa na kutaniko la angalau Wanafunzi wa Biblia kumi jijini Skien.
Knud alipoambiwa na mtu wa ukoo kuhusu kutaniko hilo dogo jijini Skien, alirudi Norway mwaka wa 1904 kumtafuta Ingebret. Alisimama barabarani na kumuuliza mwanamume fulani, “Je, unamfahamu Ingebret Andersen?” Mwanamume huyo akajibu, “Ndiyo, ni mimi.” Knud alisisimka sana hivi kwamba alifungua mkoba wake papo hapo katikati ya barabara, na akaanza kumwonyesha Ingebret vitabu alivyokuwa navyo. Ingebret naye alifurahi kukutana na Knud na kuona machapisho hayo mengi.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 92]
Kutaniko la Skien mwaka wa 1911, pamoja na Ingebret na Berthe Andersen
-