-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kazi ya kuhubiri nchini Norway ilipata nguvu zaidi mwaka wa 1903 wakati makolpota (wahubiri wa wakati wote) watatu wenye bidii walipofika kusaidia. Watatu hao walikuwa Fritiof Lindkvist, Viktor Feldt, na E. R. Gundersen.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwishoni mwa mwaka wa 1903, Ndugu Gundersen alipokuwa anahubiri eneo la Trondheim, alizungumza na Lotte Holm, ambaye alikubali machapisho. Baadaye mwanamke huyo alienda nyumbani huko Narvik, eneo lililo juu ya Mzingo wa Aktiki, na akawa mhubiri wa kwanza kaskazini mwa Norway. Baada ya hapo, Viktor Feldt alienda Narvik, akawahubiria wanaume fulani wawili na wake zao, na wote wakawa Wanafunzi wa Biblia. Walimtafuta Lotte na baada ya muda mfupi, wakawa wanakutana pamoja kujifunza Biblia. Hallgerd, dada ya Lotte, pia alikubali kweli na baadaye wote wawili wakawa mapainia wenye bidii katika sehemu mbalimbali nchini Norway.
Ndugu Feldt na Gundersen walikuwa na matokeo mazuri sana walipohubiri Bergen mwaka wa 1904 na 1905. Gazeti la Zion’s Watch Tower la Machi 1, 1905 liliripoti hivi: “Mhubiri mashuhuri wa kanisa la Free Mission la [Bergen] amesadikishwa kabisa na nuru iliyo wazi, na sasa anawaeleza wengine kuhusu Injili yote na iliyo ya kweli.”
-