-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwishoni mwa mwaka wa 1903, Ndugu Gundersen alipokuwa anahubiri eneo la Trondheim, alizungumza na Lotte Holm, ambaye alikubali machapisho. Baadaye mwanamke huyo alienda nyumbani huko Narvik, eneo lililo juu ya Mzingo wa Aktiki, na akawa mhubiri wa kwanza kaskazini mwa Norway. Baada ya hapo, Viktor Feldt alienda Narvik, akawahubiria wanaume fulani wawili na wake zao, na wote wakawa Wanafunzi wa Biblia. Walimtafuta Lotte na baada ya muda mfupi, wakawa wanakutana pamoja kujifunza Biblia. Hallgerd, dada ya Lotte, pia alikubali kweli na baadaye wote wawili wakawa mapainia wenye bidii katika sehemu mbalimbali nchini Norway.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 94]
Hallgerd Holm (1), Theodor Simonsen (2), na Lotte Holm (3)
-