-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mmoja wa kichwa cha familia ni Arnulf Jensen, mpwa wa Dag, aliyebatizwa mwaka wa 1947. Alifanya kazi ya uvuvi, na katikati ya juma alienda baharini kwa siku kadhaa kuvua samaki akitumia mashua yake. Lakini kila Ijumaa jioni, alirudi nyumbani, hata kama samaki walikuwa wengi na wavuvi wengine wangetaka kuendelea kuvua ili wapate pesa nyingi zaidi. Arnulf alihakikisha kwamba alikuwa nyumbani mwishoni mwa juma ili kuhudhuria mikutano na kushiriki katika kazi ya kuhubiri pamoja na mke wake na watoto wao wanane, ambao wote walichukua msimamo imara kwa ajili ya kweli. Mara nyingi, siku za Jumamosi na Jumapili, akina ndugu walitimiza utume wao wa kuwa “wavuvi wa watu,” wakitumia mashua ya Arnulf kufanya kazi ya uvuvi wa kiroho katika maeneo ya mbali.—Marko 1:16-18.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 133]
Mara nyingi mashua ya Arnulf ilitumiwa kwa ajili ya utumishi
-