-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mmoja aliyependezwa sana na ujumbe wa Solveig ni seremala anayeitwa Dag Jensen wa kijiji cha Hennes katika eneo la Vesterålen. Kwa miaka mingi alipata machapisho yetu kutoka kwa watu wengine waliopendezwa. Solveig alipokutana naye, alifanya mipango ili Dag apate andikisho la magazeti yetu, kisha akaenda kuhubiri katika maeneo mengine. Dag alianza kuhubiri akiwa peke yake na kuwaazima machapisho watu waliopendezwa.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwa mfano, Solveig alimweleza Andreas kuhusu Dag Jensen wa Hennes na Frits Madsen wa kisiwa cha Andøya.
Alipokutana na Dag mara ya kwanza mwaka wa 1940, “alikuwa ananyoa ndevu na uso wake ulijaa sabuni,” asema Andreas. “Sitasahau kamwe macho yake yaliyong’aa. Alisahau kabisa kwamba alikuwa ananyoa.” Andreas alimsaidia Dag kufanya maendeleo ya kiroho. Dag alikuwa na bidii sana na punde si punde, akamsaidia mke wake Anna, wengi wa rafiki zake, na pia watu wa ukoo, kujifunza kweli.
-