-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ndugu Feldt na Gundersen walikuwa na matokeo mazuri sana walipohubiri Bergen mwaka wa 1904 na 1905. Gazeti la Zion’s Watch Tower la Machi 1, 1905 liliripoti hivi: “Mhubiri mashuhuri wa kanisa la Free Mission la [Bergen] amesadikishwa kabisa na nuru iliyo wazi, na sasa anawaeleza wengine kuhusu Injili yote na iliyo ya kweli.”
Mhubiri huyo alikuwa Theodor Simonsen, ambaye baadaye alifukuzwa kutoka Kanisa la Free Mission kwa sababu ya kufundisha kweli nzuri mpya ambazo alijifunza katika machapisho yetu. Hata hivyo, Wanafunzi wa Biblia walimkaribisha Ndugu Simonsen. Watu wa Yehova walimpenda Theodor sana na pia alikuwa msemaji mzuri. Mwishowe, Ndugu Theodor aliamua kuishi Kristiania ambapo kulikuwa na kutaniko lililokuwa likiongezeka.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Alipomsikia Theodor Simonsen katika kanisa la Free Mission akisema mambo aliyokuwa amesoma katika mojawapo ya vitabu vya Wanafunzi wa Biblia, alivutiwa sana na akaanza kusoma vitabu hivyo.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa za 95, 96]
Alijitolea Kabisa Kumtumikia Yehova
THEODOR SIMONSEN
ALIZALIWA 1864
MWANAFUNZI WA BIBLIA TANGU 1905
MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Awali alikuwa mhubiri wa kanisa la Free Mission lakini baadaye akawa mwangalizi anayesafiri.
◼ THEODOR aliposoma machapisho yetu na kutambua kwamba fundisho la moto wa mateso linapingana na Biblia, alianza kufunua uwongo wa fundisho hilo kupitia hotuba zake katika kanisa la Free Mission—jambo lililowafurahisha wengi waliohudhuria. Lakini siku moja, baada ya kutoa hotuba fulani, alipewa karatasi iliyoandikwa, “Hiyo ndiyo hotuba yako ya mwisho hapa!”
Theodor alitoa hiyo hotuba ya mwisho katika kanisa la Free Mission mwaka wa 1905, na akawa Mwanafunzi wa Biblia mwaka huohuo. Baadaye, alitoa hotuba nyingi kwa mamia ya Wanafunzi wa Biblia waliozithamini sana. Theodor alifanya kazi ya kupaka nyumba rangi ili kuitegemeza familia yake kifedha huku akitumia miisho-juma kuhubiri na kufundisha. Kwa kuwa alikuwa mtulivu, mwenye ujuzi mwingi wa Biblia, na alitoa hoja zake kwa njia yenye kueleweka, Theodor alithibitika kuwa mwalimu stadi. Pia, alikuwa na sauti nzuri ya kuimba na kwa kawaida alianza na kumaliza hotuba zake kwa kuimba huku akipiga zeze.
Mwaka wa 1919, hali ya familia yake iliporuhusu, alianza kutumika akiwa mwangalizi anayesafiri. Alitumika katika mgawo huo hadi mwaka wa 1935, akitembelea makutaniko huko Norway, Denmark, na Sweden. Ilikuwa kazi ya kuchosha iliyohusisha kutia moyo makutaniko na vikundi vilivyo mbali na pia kutoa hotuba katika miji ambayo haikuwa na Wanafunzi wa Biblia. Kwa mfano: Wakati wa safari moja ya miezi 12, alipaswa kutembelea maeneo 190 kati ya Kristiansand iliyo upande wa kusini na Tromsø iliyo upande wa kaskazini. Siku hizo, waangalizi wanaosafiri walikaa mahali fulani kwa siku moja au mbili tu kisha wakaondoka na kwenda kwingine kwa kutumia aina yoyote ya usafiri uliopatikana.
Hata ingawa hakukuwa na Wanafunzi wa Biblia katika sehemu nyingi alizotembelea, watu wengi wenye kupendezwa walijitokeza alipotoa hotuba. Kwa mfano, alipotembelea Bodø mwaka wa 1922, alihubiri na kuwaalika watu kwa hotuba ya watu wote akiwa pamoja na Anna Andersen, painia ambaye pia alikuwa ametembelea eneo hilo. Johan na Olea Berntsen, waliokuwa miongoni mwa waliosikiliza hotuba yake, walipendezwa sana. Baada ya hotuba waliwaalika Theodor na Anna nyumbani kwao ili kujibu maswali yao ya Biblia. Kwa sababu hiyo, familia ya Berntsen wakawa Wanafunzi wa kwanza wa Biblia huko Bodø.
Sauti ya Theodor ilitumiwa katika hotuba zilizorekodiwa katika Kinorway kwenye gramafoni miaka ya 1930. Alitumika kwa uaminifu hadi alipokufa mwaka wa 1955 akiwa na tumaini la kwenda mbinguni.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 94]
Hallgerd Holm (1), Theodor Simonsen (2), na Lotte Holm (3)
-