-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Olaf Skau, aliyebatizwa mwaka wa 1923 alikuwa mmoja wa wahubiri katika eneo hilo. Aliwekwa rasmi kuwa mwelekezi wa utumishi kutanikoni mwaka wa 1927 na kwa miaka mingi alitumika akiwa mwangalizi mwenye kujali na ambaye alitafuta njia za kuboresha huduma. Alipanga kazi jijini Oslo na pia akapanga safari za miisho-juma za kwenda kuhubiri nje ya jiji kwa basi au lori. Alikaa macho hadi usiku wa manane akichora ramani na kupanga safari za utumishi.
Wahubiri kutoka Oslo walihubiri pia katika miji, majiji na maeneo ya mashambani. Walihubiri Halden, Fredrikstad, Hamar, Kongsvinger, Drammen, na Hønefoss. Kwa kawaida, walifika kwenye eneo saa 3 asubuhi na kuhubiri nyumba kwa nyumba mchana kutwa. Mara nyingi walifanya mikutano pia. Utendaji huo ulisaidia kuanzisha vikundi na makutaniko mapya na ulithaminiwa sana na ndugu na dada wachache walioishi katika maeneo hayo. Katika mojawapo ya kampeni hizo mwaka wa 1935, wahubiri 76 kutoka Oslo waliwaachia watu vijitabu 13,313, wastani wa vijitabu zaidi ya 175 kwa kila mhubiri!
Esther, mke wa Olaf aliugua ugonjwa wa yabisi na alitumia kiti cha magurudumu. Licha ya hayo, nyumba yao haikukosa wageni. Kwa kawaida, Olaf ndiye aliyepika na alitambulika sana kwa upishi bora wa mabawa ya kuku. Lakini, Mashahidi wengi wanakumbuka zaidi mambo yenye kujenga kiroho, mazungumzo ya Biblia yenye kusisimua, na maswali ya Biblia waliyokuwa nayo nyumbani mwa Ndugu Skaus. “Sikuzote tuliondoka kwake tukiwa tumejengwa kiroho,” asema Ragnhild Simonsen.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 109]
Olaf Skau
-