-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ndugu Feldt na Gundersen walikuwa na matokeo mazuri sana walipohubiri Bergen mwaka wa 1904 na 1905. Gazeti la Zion’s Watch Tower la Machi 1, 1905 liliripoti hivi: “Mhubiri mashuhuri wa kanisa la Free Mission la [Bergen] amesadikishwa kabisa na nuru iliyo wazi, na sasa anawaeleza wengine kuhusu Injili yote na iliyo ya kweli.”
Mhubiri huyo alikuwa Theodor Simonsen, ambaye baadaye alifukuzwa kutoka Kanisa la Free Mission kwa sababu ya kufundisha kweli nzuri mpya ambazo alijifunza katika machapisho yetu. Hata hivyo, Wanafunzi wa Biblia walimkaribisha Ndugu Simonsen. Watu wa Yehova walimpenda Theodor sana na pia alikuwa msemaji mzuri.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1905 hivi, kulikuwa na makutaniko ya Wanafunzi wa Biblia katika majiji manne, yaani, Skien, Kristiania, Bergen, na Narvik.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Dada painia wa kwanza alikuwa Helga Hess. Alikuwa yatima aliyeishi jijini Bergen, ambapo alianza kufundisha watoto mambo ya dini katika shule ya Jumapili akiwa na umri wa miaka 17. Alipomsikia Theodor Simonsen katika kanisa la Free Mission akisema mambo aliyokuwa amesoma katika mojawapo ya vitabu vya Wanafunzi wa Biblia, alivutiwa sana na akaanza kusoma vitabu hivyo. Akaacha kazi, na mwaka wa 1905, akiwa na umri wa miaka 19, akaenda kuhubiri habari njema jijini Hamar na Gjøvik.
-