-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa za 95, 96]
Alijitolea Kabisa Kumtumikia Yehova
THEODOR SIMONSEN
ALIZALIWA 1864
MWANAFUNZI WA BIBLIA TANGU 1905
MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Awali alikuwa mhubiri wa kanisa la Free Mission lakini baadaye akawa mwangalizi anayesafiri.
-
-
Norway2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1919, hali ya familia yake iliporuhusu, alianza kutumika akiwa mwangalizi anayesafiri. Alitumika katika mgawo huo hadi mwaka wa 1935, akitembelea makutaniko huko Norway, Denmark, na Sweden. Ilikuwa kazi ya kuchosha iliyohusisha kutia moyo makutaniko na vikundi vilivyo mbali na pia kutoa hotuba katika miji ambayo haikuwa na Wanafunzi wa Biblia. Kwa mfano: Wakati wa safari moja ya miezi 12, alipaswa kutembelea maeneo 190 kati ya Kristiansand iliyo upande wa kusini na Tromsø iliyo upande wa kaskazini. Siku hizo, waangalizi wanaosafiri walikaa mahali fulani kwa siku moja au mbili tu kisha wakaondoka na kwenda kwingine kwa kutumia aina yoyote ya usafiri uliopatikana.
Hata ingawa hakukuwa na Wanafunzi wa Biblia katika sehemu nyingi alizotembelea, watu wengi wenye kupendezwa walijitokeza alipotoa hotuba. Kwa mfano, alipotembelea Bodø mwaka wa 1922, alihubiri na kuwaalika watu kwa hotuba ya watu wote akiwa pamoja na Anna Andersen, painia ambaye pia alikuwa ametembelea eneo hilo. Johan na Olea Berntsen, waliokuwa miongoni mwa waliosikiliza hotuba yake, walipendezwa sana. Baada ya hotuba waliwaalika Theodor na Anna nyumbani kwao ili kujibu maswali yao ya Biblia. Kwa sababu hiyo, familia ya Berntsen wakawa Wanafunzi wa kwanza wa Biblia huko Bodø.
-