Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • WATOTO WANAOMLETEA SIFA MUUMBA WAO

      Kwa kufuata kwa ujasiri dhamiri zao zilizozoezwa na Biblia, watoto wengi huko Papua New Guinea wametoa ushahidi mzuri. Kwa mfano, mapema katika mwaka wa 1966, mwalimu mmoja wa shule ya msingi aliwaambia watoto saba wa Mashahidi wa eneo hilo kwamba walipaswa kusalimu bendera wakati wa sherehe ambazo zingefanywa juma lililofuata. Siku hiyo ilipofika, watoto wote saba walikataa kusalimu bendera mbele ya wanafunzi 300 hivi. Kwa sababu hiyo, walifukuzwa shuleni, hata ingawa wazazi wao walikuwa wameandika barua wakiomba watoto wao wasihusishwe katika sherehe hizo. Mzee mmoja kutoka kutaniko la huko aliandika barua kwa maofisa wa serikali huko Papua New Guinea na Australia kuhusu jambo hilo.

      Mnamo Machi 23, Msimamizi wa Serikali ya Australia huko Papua New Guinea aliwapigia simu wakuu wa shule hiyo na kuagiza kwamba watoto hao warudishwe shuleni mara moja. Ibada ya kweli ilikuwa imepata ushindi mdogo wa kisheria. Leo, serikali ya Papua New Guinea inaendelea kuheshimu haki ya watoto ya kukataa kusalimu bendera kwa sababu ya dhamiri.

      “Watoto na wanaonyonya” wanaweza kumsifu Yehova katika njia nyingine pia. (Mt. 21:16) Fikiria mfano wa Naomi kutoka sehemu za mlimani ambaye wazazi wake, Joe na Helen, hawakuwa Mashahidi. Naomi alipokuwa na umri wa miaka mitatu hivi, aliishi kwa mwaka mmoja hivi na shangazi yake, yaani dada ya Helen, ambaye ni Shahidi mwenye bidii huko Lae. Shangazi yake alikuwa akimbeba Naomi ndani ya mfuko ulioning’inizwa kwenye bega lake kila mara alipoenda mahubiri. Kwa njia hiyo, Naomi alijua tumaini la Ufalme, na pia shangazi yake alitumia sana picha katika Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.

      Naomi aliporudi kwa wazazi wake, alichukua kichapo cha Mashahidi, akatoka nje ya nyumba, na kubisha mlango wao kwa sauti ya juu. “Ingia ndani,” wazazi wake wakamwambia. Alipoingia tena ndani, msichana huyo mdogo alisema hivi: “Habari. Mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, na nimekuja kuzungumza nanyi kuhusu Biblia.” Huku Joe na Helen wakimtazama kwa mshangao, Naomi aliendelea kusema: “Biblia inasema kwamba Paradiso itakuwa juu ya dunia; na Mfalme mmoja, Yesu, atatawala juu yetu. Kila kitu kinachotuzunguka kimefanywa na Yehova.”

      Joe na Helen walipigwa na butwaa. “Jamani majirani wetu watasema nini!” Joe akamwambia mke wake. “Tafadhali kesho mfungie ndani.”

      Siku iliyofuata, wazazi wake walipokuwa wameketi nje ya nyumba yao, Naomi aligonga kwa sauti ukuta wa chumba chake cha kulala. “Njoo huku nje,” Joe akamwambia. Naomi alitoka na kuanzisha mazungumzo: “Habari. Mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, na nimekuja kukuhubiria. Watu wazuri wataishi milele duniani. Lakini watu ambao hukasirika na kufanya mambo mabaya hawataishi katika Paradiso.” Wakiwa wamechanganyikiwa, Helen alianza kulia, huku Joe akiondoka kwa hasira kwenda kulala.

      Usiku huo, kwa sababu ya udadisi, Joe alianza kusoma Biblia yake nzee ya tafsiri ya King James Version na akapata jina Yehova. Asubuhi iliyofuata, badala ya kwenda kazini, aliwaandikia Mashahidi barua kisha akasafiri kwa gari umbali wa kilomita 40 ili kuipeleka kwenye Jumba la Ufalme huko Mlima Hagen.

      Akina ndugu waliwatembelea Joe na Helen na kupanga kuanza kujifunza nao Biblia kwa ukawaida. Pia walimfundisha Helen kujua kusoma. Hatimaye, wote wawili, Joe na Helen walibatizwa, na Helen aliwafundisha wanafunzi wengine wa Biblia kujua kusoma. Yote hayo kwa sababu msichana mdogo alimsifu Yehova!

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 145]

      Baadhi ya watoto waliofukuzwa shuleni kwa kukataa kusalimu bendera

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki