Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • MAKUSANYIKO YASIYOSAHAULIKA

      Mnamo Julai 1955, John Cutforth, mmishonari Mkanada aliyekuwa akitumika huko Australia, aliwasili Port Moresby na kuwa mwangalizi wa kwanza wa mzunguko. Mara moja, John alipenda eneo hilo, utamaduni, na watu wake. Hakujua kwamba angetumika nchini Papua New Guinea kwa zaidi ya miaka 35.

      John alifika akiwa na sinema inayoitwa The New World Society in Action, masimulizi yaliyoonyesha utaratibu wa tengenezo na makusanyiko ya Mashahidi wa Yehova. Wakati wa ziara yake ya majuma matatu, alionyesha sinema hiyo mara 14 nyakati nyingine mbele ya mamia ya wahudhuriaji au hata mbele ya watu 2,000 hivi. Watu wengi sana waliifurahia, hiyo ikiwa mara ya kwanza kwa wengine wao kutazama sinema yoyote.

      Ziara ya John ilifikia mwisho wakati wa kusanyiko la mzunguko la siku moja huko Haima. “Wanaotaka kubatizwa walipoombwa wasimame, . . . watu 70 walisimama!” anakumbuka Tom Kitto. “Mioyo yetu ilijawa na shangwe tulipoona ndugu 40 na dada 30 wakisimama msituni kwenye ukingo wa mto wakiwa tayari kuonyesha wakfu wao kwa Yehova.”

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • KUTUMIA PICHA KUHUBIRI

      Mnamo 1957, John Cutforth alihamia kabisa Papua New Guinea na kuwa mwangalizi anayesafiri huko. Tangu ziara yake ya kwanza, alikuwa amefikiria sana njia bora zaidi ya kuwahubiria wenyeji, kwa kuwa wengi wao hawakujua kusoma na kuandika. Sasa alikuwa tayari kutumia mbinu yake.

      Alipokuwa akitoa hotuba mbele ya kutaniko au kikundi cha mbali, John aliandika jina lake na la mtafsiri kwenye ubao mweusi. Kisha, akaelekeza kidole mbinguni, na kuwauliza wasikilizaji, “Mungu, jina lake nani?” Akaandika jibu lao, “Yehova” na “Zaburi 83:18” juu ya ubao huo. Chini yake upande wa kushoto, aliandika kichwa “Ulimwengu wa Kale” na kuchora wanaume wawili wakipigana, mtu akilia, kaburi, na “Waroma 5:12.” Upande wa kulia, akaandika kichwa “Ulimwengu Mpya” na kuchora wanaume wawili wakisalimiana kwa mikono, mtu akitabasamu, kaburi lililofutwa, na “Ufunuo 21:4.” Baadaye, alitoa hotuba yenye kusisimua ili kueleza michoro yake. Kisha akawakaribisha wasikilizaji wasimame mbele na kurudia hotuba yake. Walipokuwa wameelewa, aliwaambia wachore picha hizo kwenye karatasi na kuzitumia katika kazi ya kuhubiri.

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 91]

      Alipendwa na Watu Wengi

      Alipokuwa akitumika akiwa mmishonari huko Papua New Guinea, John Cutforth alipendwa na watu wengi. Hebu ona mambo ambayo baadhi ya wamishonari wenzake na wengine waliotumika pamoja naye walisema kumhusu.—Met. 27:2.

      Erna Andersson: “John alituambia hivi: ‘Mmishonari halisi huwa mambo yote kwa watu wa namna zote. Ikiwa watu wanakukaribisha uketi kwenye kisiki cha mti, keti, hawana kiti kingine bora kuliko hicho. Wakikupa kitanda kilichotengenezwa kwa njia isiyopendeza sana, kubali na ukilalie, kimetengenezwa kwa fadhili. Wakikupa chakula kisicho cha kawaida, kula, kwa sababu kimetayarishwa kwa upendo.’ John aliweka mfano bora sana wa mmishonari mwenye kujidhabihu.”

      Awak Duvun: “Wakati wa utawala wa wakoloni, John aliwafundisha watu kihalisi kwamba hakupaswi kuwa na ubaguzi kati ya watu weusi na weupe! Mara nyingi alisema, ‘Hakuna tofauti kati ya mtu mweusi na mzungu!’ Aliwapenda watu wote.”

      Peter Linke: “Alasiri moja, baada ya kusafiri mchana kutwa, John alifika nyumbani kwetu Goroka, akiwa amejawa na vumbi na uchovu. Lakini baada ya chakula cha jioni akasema, ‘Sijamsaidia mtu yeyote leo’ kisha akatoka nje na kutokomea kwenye giza la jioni na kwenda kuitembelea familia moja ili kuwatia moyo. Sikuzote aliwafikiria wengine. Sote tulimpenda.”

      Jim Dobbins: “John alitufunza jinsi ya kuishi maisha rahisi na kufundisha kwa njia rahisi, kwa kutumia mifano ambayo watu wangeweza kuelewa kama vile Yesu alivyofanya. Tulipofanya hivyo tuliweza kuwasiliana na wale ambao hawakujua kusoma na kuandika.”

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 87]

      John Cutforth

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 90]

      Kulia: John Cutforth akifundisha kwa kutumia picha; chini: ndugu akibeba ubao wenye picha ili akahubiri katika vijiji vya mbali

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki