-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kora Leke alitumia uchawi na miti-shamba kuwatibu wagonjwa. Hata hivyo, alipoanza kujifunza Biblia, alijitahidi sana kuacha roho aliyekuwa akimsaidia katika uchawi wake. Kama Soare, Kora alikuwa ameazimia kuachana na roho waovu, na alifaulu kwa msaada wa Yehova. Baadaye, alitumika akiwa painia wa kawaida na kisha painia wa pekee. Hata sasa ingawa yeye ni mzee na miguu yake ni dhaifu, ndugu huyo mshikamanifu anaendelea kuwaeleza jirani zake habari njema.
Kora alifika kwa njia gani mahali ambapo alipenda kukaa akihubiri? Akina ndugu walimpeleka kwa toroli (wheelbarrow) ambayo ndiyo iliyokuwa njia pekee iliyofaa wakati huo. Baadaye, ndugu fulani mbunifu katika ofisi ya tawi alimtengenezea kiti cha magurudumu akitumia kiunzi kilichotengenezwa kwa chuma cha kiti cha kawaida, magurudumu ya baiskeli, na chandarua. Kora angeweza kujisukuma mwenyewe kwa kiti hicho kipya na amekitumia kikamili! Wazee kama yeye ni kielelezo chenye kuchochea kama nini, kwani wanaufurahisha sana moyo wa Yehova!—Met. 27:11.
-
-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 135]
Soare Maiga
-