-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Soare Maiga aliishi katika kijiji kilichokuwa kilomita 50 hivi kutoka Port Moresby na aliogopwa sana kwa sababu ya nguvu zake za kiuchawi. Hata hivyo, alitaka sana kujua kuhusu imani ya Mashahidi wa Yehova, kwa hiyo alijiunga na kikundi kimoja kilichokuwa kikijifunza Biblia. Punde si punde, alikubali kweli na akaacha mazoea yake ya zamani. Lakini kila mara alipojaribu kutupa vitu vyake vya kuwasiliana na pepo, vitu hivyo vilirudi kwa njia ya ajabu! Hata hivyo, Soare alikuwa ameazimia ‘kumpinga Ibilisi,’ kwa hiyo siku moja alitia vitu hivyo ndani ya mkoba, akatia jiwe ndani ya mkoba huo, kisha akaenda huko Port Moresby na kuutupa baharini. (Yak. 4:7) Vitu hivyo havikurudi tena. Baada ya hilo, mtu huyo jasiri akawa Shahidi mwenye bidii wa Mungu wa kweli, Yehova.
-
-
Papua New Guinea2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 135]
Kora Leke
-