Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • “NJOO UWAFUNDISHE WATU WANGU”

      Mapema katika mwaka wa 1952, Bobogi Naiori, chifu wa eneo la Koiari ambaye pia alikuwa mchawi maarufu, alimtembelea Heni Heni, kwani alikuwa wantok wake, au mtu wa kabila lake, na akahudhuria mkutano katika nyumba yake. Kwa kuwa alivutiwa na mambo aliyoona na kusikia, baadaye Bobogi alimwendea Tom Kitto na kumsihi: “Tafadhali, njoo uwafundishe watu wangu kuhusu kweli!”

      Muda mfupi baadaye, Tom na Rowena walisafiri kwa gari lao kuukuu kupitia barabara za udongo kufika nyumbani kwa Bobogi huko Haima, kijiji kidogo kilicho umbali wa kilomita 25 hivi kaskazini ya Port Moresby. Tom aliwahubiria wanakijiji waliokuwa wamekusanyika na Bobogi akatafsiri. Kuanzia wakati huo, watu 30 hivi wakaanza kujifunza Biblia.

      Baadaye katika mwezi huo, kikundi kilichokuwa huko Haima kilijenga jumba dogo kwa ajili ya mikutano ya Kikristo. “Jumba hilo lilikuwa na kiunzi cha mbao, paa lililoezekwa kwa nyasi, na kuta zilizofika kiunoni zilizofumwa kwa mianzi,” anakumbuka Elsie Horsburgh ambaye baadaye alihudhuria mikutano huko. “Ndani kulikuwa tu na viti vya mbao, taa ya mafuta, na ubao mweusi mdogo.” Jengo hilo la hali ya chini likawa Jumba la Ufalme la kwanza nchini Papua New Guinea.

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 85]

      Jumba la Ufalme la kwanza nchini huko Haima, Port Moresby

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki