Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mnamo 1957, David Walker, ndugu Mwaustralia mwenye umri wa miaka 26 aliyekuwa akiishi huko Port Moresby, alisikia kwamba watu katika kijiji jirani cha Manu Manu na katika eneo la Gabadi walikuwa wanapendezwa na kweli. David aliacha kazi yake, akaanza kufanya upainia wa pekee, na akahubiri katika eneo hilo kwa mwaka mzima akiwa peke yake. Wengine waliendeleza alipoachia, na sasa kuna kutaniko na Jumba la Ufalme huko Manu Manu.

      Wakati huohuo, Don Fielder alikutana na wavuvi kadhaa waliopendezwa na kweli alipokuwa akihubiri kwenye soko la Koki huko Port Moresby. Wanaume hao walikuja kutoka Hula, kijiji cha pwani karibu kilomita 100 upande wa mashariki. Ili kuwasaidia wao na familia zao, Don, pamoja na Athol (Dap) Robson na watu wengine wenye kupendezwa waliokuwa wenyeji wa Hula, walielekea huko kwa kutumia mtumbwi mpya wa Don wenye urefu wa mita 8. Walikaa huko Hula kwa siku tatu na kuanzisha kikundi kidogo cha kujifunza.

      Muda mfupi baadaye, Don alihamia Hula na akatumika akiwa painia wa pekee pamoja na mke wake Shirley, na binti yao Debbie mwenye umri wa miaka miwili. “Tulijenga nyumba ndogo na kuanza kuhubiri katika vijiji vitano vya eneo hilo,” anaeleza Don. “Hilo lilihusisha kutembea umbali wa kilomita 12 kwenda na kurudi kila siku. Ilikuwa kazi yenye kuchosha lakini ilituburudisha kiroho kwani tulianzisha mafunzo mengi ya Biblia na punde tukawa na wahubiri wapya wanane waliohubiri pamoja nasi.”

      Kazi ya kuhubiri ya Don na Shirley ilimkasirisha sana kasisi wa Kanisa la United la eneo hilo, ambaye alimshinikiza mwenye shamba awaamuru waondoe nyumba yao kutoka kwenye shamba lake. “Watu wa kijiji cha karibu waliposikia jambo hilo, walikasirika sana kwa sababu hawakutaka tuondoke,” anasema Don. “Watu 20 hivi walitusaidia kuhamisha nyumba yote kutia ndani msingi wake, hadi kwenye shamba lingine lililokuwa la kijiji chao.”

      Kasisi huyo aliyekasirika hakukata tamaa. Alijitahidi kuwashinikiza wenye mamlaka wa Port Moresby watupige marufuku tusijenge nyumba yetu popote katika wilaya hiyo. “Badala ya kuondoka katika mgawo wetu,” anasema Don, “tulimwomba Alf Green, fundi stadi wa mbao, achukue mbao za nyumba hiyo yetu na kujenga chumba kidogo juu ya mtumbwi wetu. Kisha tukatia nanga katika kinamasi cha mikoko karibu na mlango wa mto uliokuwa karibu. Tuliishi na kufanya upainia tukiwa mahali hapo penye mbu wengi na mamba kwa miaka miwili na nusu iliyofuata.” Binti yao wa pili Vicki alipozaliwa, Don na familia yake walirudi Port Moresby.

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Punde tu baada ya hapo, Waaustralia wawili vijana, Jim Smith na Lionel Dingle, walipewa mgawo wa kwenda Kerema kuwa mapainia wa pekee. Mara moja walianza kujifunza Kitairuma, lugha ya eneo hilo. “Tulisema neno katika lugha ya Motu, na wanafunzi wetu wa Biblia walituambia neno linalopatana nalo katika Kitairuma nasi tukaliandika,” anaeleza Jim. “Kwa njia hiyo, tulikuwa na maneno kadhaa ambayo yalitusaidia kufanyiza msamiati uliotusaidia kutoa utangulizi rahisi wa habari za Biblia. Watu wa eneo hilo walishangaa kutusikia tukizungumza lugha yao, kwa kuwa hakuna mzungu yeyote katika wilaya yote ambaye angeweza kufanya hivyo. Baada ya miezi mitatu tulikuwa tukiongoza mikutano ya kila juma katika Kitairuma pande zote za Ghuba ya Kerema.”

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • KUKABILIANA NA MADHEHEBU YA WAABUDU-MALI

      Mnamo 1960, mapainia wa pekee wengine wawili kutoka Australia, Stephen Blundy na Allen Hosking, walihamia kijiji cha Savaiviri kilichoko kilomita 50 hivi mashariki ya Kerema. Baada ya kuishi katika hema kwa miezi mitatu, Stephen na Allen walihamia katika nyumba ndogo ya msituni iliyokuwa katika shamba la minazi lililozungukwa na kinamasi kikubwa.

      Savaiviri lilikuwa eneo linalojulikana sana kwa sababu ya madhehebu yake ya waabudu-mali. Madhehebu hiyo ilianza jinsi gani? Wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu, wenyeji walistaajabishwa na utajiri, au mali, ambazo askari-jeshi wageni walikuwa nazo. Kisha vita vilikwisha, na wanajeshi wakafunga virago vyao na kuondoka. Wanakijiji fulani walisema kwamba kwa kuwa mali hizo zilikuwa zimetoka mbali sana mahali wasipoweza kuona—kwa kuwa wanaamini kuwa pepo wanaishi mahali pasipoonekana—basi mababu zao waliokufa walikuwa wakiwatumia mali hizo lakini wanajeshi hao ndio waliokuwa wakizuia. Ili kuwajulisha pepo uhitaji wao, watu waliigiza vita na kujenga gati zenye nguvu ili kujitayarishia kwa ajili ya siku hiyo tukufu wakati ambapo mali mpya zingefika.

      Baada ya muda, Stephen na Allen walikuwa wakijfunza na washiriki 250 hivi wa madhehebu hiyo, kutia ndani kiongozi wao na baadhi ya “mitume kumi na wawili” wake. “Wengi kati ya watu hao walikubali kweli,” anasema Stephen. “Kwa kweli, ofisa mmoja wa serikali alituambia baadaye kwamba kazi yetu ya kuhubiri iliwasaidia sana kumaliza madhehebu hiyo ya waabudu-mali huko Savaiviri.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki