Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kwa mfano, karibu na mwaka wa 1970, ofisi ya tawi ilianza kupokea ripoti za utumishi wa shambani kutoka kwa mtu asiyejulikana, aliyekuwa katika kutaniko lisilojulikana, na katika kijiji kisichojulikana kwenye Mto Sepik ulio mbali sana. Ofisi ya tawi ilimwomba Mike Fisher, mwangalizi wa mzunguko, achunguze jambo hilo.

      “Ili kufika kwenye kijiji hicho, nilisafiri saa kumi kwa mtumbwi wenye injini kupitia mto mwembamba uliopita katikati ya msitu uliojaa mbu,” anaeleza Mike. “Mwishowe, nilifika jioni sana, na nikakutana na mtu huyo aliyekuwa ametengwa na ushirika miaka mingi mapema katika eneo lingine. Alirudi katika kijiji chake, akatubu dhambi zake, na kuanza kuwahubiria watu. Zaidi ya watu 30 katika kijiji hicho walijiita Mashahidi wa Yehova na wengine wao walistahili kubatizwa. Muda mfupi baadaye, mtu huyo aliyetubu alirudishwa, na kikundi hicho kikatambuliwa rasmi na ofisi ya tawi.”

      Katika mwaka wa 1992, mwangalizi mwingine wa mzunguko, Daryl Bryon, aligundua kwamba kuna kijiji fulani cha mbali ambako ilisemekana kuwa watu wanapendezwa na kweli. “Ili kufika kwenye kijiji hicho, nilisafiri kwa gari kwa kilomita 80, nikatembea katika msitu mkubwa kwa saa nzima na nusu, kisha nikasafiri kwa mtumbwi nikipiga makasia dhidi ya mkondo wa maji kwa saa nyingine moja,” Daryl anaeleza. “Nilishangaa sana kuona kwamba kwenye ukingo wa mto, katikati ya milima mirefu, kulikuwa na jengo jipya lenye ubao uliosema ‘Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova.’

      “Kulikuwa na watu 25 hivi wanaopendezwa ambao walikutana katika jumba hilo kila Jumapili ili kujifunza kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Kwa kuwa walidai kuwa Mashahidi, niliwauliza ikiwa walitafuna tambuu. ‘Hapana,’ walinijibu. ‘Tuliacha kufanya hivyo mwaka mmoja uliopita tulipojifunza kweli!’ Nilifurahi kama nini wakati ofisi ya tawi ilipoongeza kikundi hicho kwenye mzunguko wangu.”

  • Papua New Guinea
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 115]

      Mike Fisher akiwa kwenye Mto Sepik

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki