Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Luka—Mfanyakazi Mwenzi Mpendwa
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 15
    • Luka—Mfanyakazi Mwenzi Mpendwa

      NI MWAKA wa 65 W.K. Mahali penyewe palikuwa Roma. Luka alijua hatari ya kujitambulisha kuwa rafiki ya mtume Paulo, ambaye wakati huo alikuwa ameshtakiwa kwa sababu ya imani yake. Ilionekana kwamba Paulo angehukumiwa kifo. Lakini wakati huo hatari, Luka peke yake ndiye aliyekuwa pamoja na mtume huyo.—2 Timotheo 4:6, 11.

      Jina Luka si geni masikioni mwa wasomaji wa Biblia kwa sababu Injili aliyoandika inaitwa kwa jina lake. Luka alifunga safari ndefu pamoja na Paulo. Paulo alimwita Luka “tabibu mpendwa” na ‘mfanyakazi mwenzi.’ (Wakolosai 4:14; Filemoni 24)

  • Luka—Mfanyakazi Mwenzi Mpendwa
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 15
    • Luka anapozungumzia matukio katika safari ya Paulo na waandamani wake kupitia Asia Ndogo, anasema hivi: “Wakapita Misia na kushuka mpaka Troa.” Wakiwa Troa Paulo alipata maono ya mwanamume Mmakedonia ambaye alisihi hivi: “Vuka uingie Makedonia utusaidie.” Luka anaongezea: “Basi mara tu alipokuwa amekwisha kuona maono hayo, tukajaribu kuingia Makedonia.” (Matendo 16:8-10) Kwa kuwa mwanzoni alisema “wakapita” na baadaye anasema “tukajaribu,” inaelekea Luka alijiunga na Paulo na wenzake huko Troa. Kisha, Luka anaeleza kuhusu kazi ya kuhubiri huko Filipi kwa njia inayoonyesha kwamba alishiriki kazi hiyo. “Siku ya sabato,” Luka anaandika, “tukatoka nje ya lango kando ya mto, ambapo tulikuwa tukifikiri kwamba palikuwa na mahali pa sala; nasi tukaketi na kuanza kusema na wanawake waliokuwa wamekusanyika.” Matokeo yalikuwa kwamba Lidia na watu wote wa nyumbani mwake walikubali habari njema na kubatizwa.—Matendo 16:11-15.

      Upinzani ulitokea huko Filipi, ambako Paulo alimponya kijakazi aliyekuwa akibashiri kwa uwezo wa “roho mwovu wa uaguzi.” Mabwana wake walipoona kwamba chanzo chao cha mapato kimeondolewa, waliwashika Paulo na Sila. Baadaye Paulo na Sila walipigwa na kutupwa gerezani. Inaelekea kwamba Luka hakukamatwa, kwa sababu hajihusishi anapoeleza mambo yaliyowapata wenzake. Walipoachiliwa, ‘Paulo na Sila waliwatia moyo akina ndugu kisha wakaondoka.’ Baadaye Luka anaanza tena kujihusisha katika masimulizi hayo wakati Paulo anaporudi Filipi. (Matendo 16:16-40; 20:5, 6) Huenda Luka alibaki Filipi ili kusimamia kazi katika eneo hilo.

      Kukusanya Habari

      Luka alipata jinsi gani habari alizoandika katika Injili yake na katika kitabu cha Matendo? Sehemu za kitabu cha Matendo ambazo Luka anajihusisha katika masimulizi, zinaonyesha kwamba Luka alisafiri na Paulo kutoka Filipi kwenda Yerusalemu, ambako mtume huyo alikamatwa tena. Wakiwa njiani, Paulo na wenzake walikaa na Filipo, yule mweneza-injili huko Kaisaria. (Matendo 20:6; 21:1-17) Luka angeweza kupata habari kuhusu kazi ya mapema ya umishonari huko Samaria kutoka kwa Filipo mwenyewe, ambaye aliongoza kazi ya kuhubiri katika eneo hilo. (Matendo 8:4-25) Lakini Luka alipata habari kutoka vyanzo gani vingine?

      Huenda miaka miwili ambayo Paulo alikaa kifungoni huko Kaisaria ilimpa Luka nafasi ya kufanya utafiti kuhusu masimulizi yake ya Injili.

  • Luka—Mfanyakazi Mwenzi Mpendwa
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Novemba 15
    • Mwandamani wa Mfungwa

      Luka alimhangaikia mtume Paulo. Paulo alipokuwa kizuizini huko Kaisaria, mtawala Mroma aliyeitwa Feliksi aliamuru kwamba ‘yeyote kati ya watu wa Paulo,’ asikatazwe “kumhudumia.” (Matendo 24:23) Inaelekea kwamba Luka alikuwa mmoja wa wahudumu hao. Kwa kuwa nyakati nyingine Paulo hakuwa na afya njema, huenda kumhudumia kulitia ndani kutunzwa na huyo “tabibu mpendwa.”—Wakolosai 4:14; Wagalatia 4:13.

      Paulo alipokata rufani kwa Kaisari, Festo mtawala Mroma alimtuma mtume huyo huko Roma. Luka aliandamana kwa ushikamanifu na mfungwa huyo aliposafirishwa kwa meli hadi Italia, naye aliandika simulizi lililo wazi kuhusu kuvunjika kwa meli yao. (Matendo 24:27; 25:9-12; 27:1, 9-44) Akiwa katika kifungo cha nyumbani huko Roma, Paulo aliandika barua kadhaa zilizoongozwa na roho, naye anamtaja Luka katika barua mbili. (Matendo 28:30; Wakolosai 4:14; Filemoni 24) Inaelekea kwamba Luka aliandika kitabu cha Matendo katika kipindi hicho cha miaka miwili.

      Hapana shaka kwamba kulikuwa na shughuli nyingi za kiroho katika nyumba ya Paulo huko Roma. Akiwa hapo, Luka angeweza kukutana na wafanyakazi wengine wenzi wa Paulo, kama vile Tikiko, Aristarko, Marko, Yusto, Epafra, na Onesimo.—Wakolosai 4:7-14.

      Paulo alipofungwa mara ya pili, wakati alipohisi kwamba kifo chake kilikuwa kimekaribia, Luka mwenye ushikamanifu na ujasiri alikuwa pamoja naye hata ingawa watu wengine walikuwa wamemwacha mtume huyo. Huenda Luka alihatarisha uhuru wake mwenyewe kwa kubaki na Paulo. Labda akitenda kama mwandishi, huenda Luka aliandika maneno haya ya Paulo: “Luka peke yake ndiye yupo pamoja nami.” Kulingana na mapokeo, Paulo aliuawa kwa kukatwa kichwa muda mfupi baadaye.—2 Timotheo 4:6-8, 11, 16.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki