-
Akila na Prisila—Wenzi Walio Kielelezo ChemaMnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 15
-
-
Kwa sababu hiyo, ilikuwa katika jiji la Kigiriki la Korintho ambapo mtume Paulo alikutana na Akila na Prisila. Paulo alipofika Korintho, Akila na Prisila walimtolea kwa fadhili ukaribishaji-wageni na pia kazi, kwa kuwa walikuwa na kazi ileile—kutengeneza-mahema.—Matendo 18:2, 3.
-
-
Akila na Prisila—Wenzi Walio Kielelezo ChemaMnara wa Mlinzi—1996 | Desemba 15
-
-
Yamkini Paulo alitumia nyumba ya Akila kuwa kitovu cha utendaji wake wa umishonari wakati wa ile miezi 18 aliyokaa Korintho. (Matendo 18:3, 11) Basi, yawezekana kwamba Akila na Prisila walikuwa na furaha ya kuwa pia na Sila (Silvano) na Timotheo wakiwa wageni-waalikwa walipofika kutoka Makedonia. (Matendo 18:5) Zile barua mbili za Paulo kwa Wathesalonike, ambazo baadaye zilikuwa sehemu ya vitabu vya Biblia vinavyokubaliwa, zaweza kuwa ziliandikwa wakati huyo mtume alipokuwa akikaa na Akila na Prisila.
Ni rahisi kuwazia kwamba wakati huo nyumba ya Prisila na Akila ilikuwa kitovu kwelikweli cha utendaji wa kitheokrasi. Labda rafiki wengi wapendwa waliizuru mara nyingi—Stefanasi na familia yake, Wakristo wa kwanza katika mkoa wa Akaya, waliobatizwa na Paulo mwenyewe; Titio Yustasi, aliyemruhusu Paulo atumie nyumba yake ili kutoa hotuba mbalimbali; na Krispo, yule ofisa-msimamizi wa sinagogi, aliyekubali kweli pamoja na wote wa nyumba yake. (Matendo 18:7, 8; 1 Wakorintho 1:16) Kisha kulikuwa na Fortunato na Akaiko; Gayo, ambaye huenda ikawa mikutano ya kutaniko ilifanyiwa nyumbani kwake; Erasto, yule mtumishi wa jiji; Tertio, mwandishi ambaye Paulo alimtumia kuwaandikia Waroma barua; na Fibi, dada mwaminifu wa kutaniko la karibu la Kenkrea, ambaye labda alibeba hiyo barua kutoka Korintho hadi Roma.—Warumi 16:1, 22, 23; 1 Wakorintho 16:17.
-